Kama Si Wewe

By Goodluck Gozbert

Lyrics

Na wala sio sababu ya jina langu 

Wala sio sababu nina-vaa 

Najua sio sababu ya sadaka zangu 

Oh, maana ndio ninashangaa 

Nilijua kwamba nimeshapoteza nafasi 

Mimi ni nani kwani? Nakosa neno kusema 

Unisamehe, sikujua unanipenda hivi 

Umefanya bure, sawa upendavyo 

Umeruhusu niwe, vile upendavyo 


Refrain:

Nitakushukuru tu, kwa neema 

Asante tu, kwa wema 

Nitakushukuru tu, kwa neema 

Asante tu, kwa wema 

Maana kama si wewe 

Kama si wewe ningekuwa wapi? 

Wacha machozi yanitirike tu 

Wacha kilio nikulilie Mungu 


Natafuta cha kunitenga nawe, bado sijaona 

Nilishakatwakatwa moyo na kupondwa na wanadamu 

Wao wataniambia nini, nikiwa nawe? 

Leo wataniambia nini, nikiwa nawe? 

Pesa huitwa sabuni, ila maji ni wewe 

Unioshe Bwana, nitakase  


Nitakushukuru tu, kwa neema 

Asante tu, kwa wema 

Maana kama si wewe 

Kama si wewe ningekuwa wapi? 

Wacha machozi yanitirike tu 

Wacha kilio nikulilie Mungu 

Goodluck Gozbert - Kama Si Wewe (Official Video ) For SKIZA sms 7630294 to 811