Msalaba ndio asili ya mema
Lyrics
Sioni haya kwa Bwana,
Kwake nitang’ara!
Mti wake sitakana,
Ni neno imara.
(Chorus)
Msalaba ndio asili ya mema,
Nikatua mzigo hapo;
Nina uzima, furaha daima,
Njoni kafurahini papo.
Kama kiti chake vivyo,
Ni yake ahadi;
Alivyowekewa navyo,
Kamwe, havirudi.
Bwana wangu, tena Mungu,
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu,
Wala kunikana.
Atakiri langu jina,
Mbele za Babaye,
Anipe pahali tena,
Mbinguni nikae
# At the Cross
"Angela chibalonza || sioni haya \/\/ msalaba\/\/ piano tutorial"
Song Information
- Artist
- Angela Chibalonza
- Released
- April 13, 2022
- Genre / Category
- swahili
- Views
- 13,907