Chorus / Description :
Jina lako Yesu lina nguvu na uweza
Wa kuvunja hila
minyororo ya shetani
Hata hili linapita
Hata hili lina mwisho
Hata hili linapita
Hata hili lina mwisho
Ni kweli napitia kipindi kigumu
Moyo wangu unauma
Nijaribu lililosima mbele zako kizito
Moyo unafadhaika
Lakini namwimini Mungu atanivusha tu
Wakati mwingine nilikumbana na hatari
Ya kugharimu uhai wangu
Mungu hakuniacha, MUngu alinibeba
Hata hili linapita, Hata hili lina ukomo wake
Kila jaribu linalokuja mbele yangu
Bibilia linasema lina mlango wa kutokea
Waswahili wanasema hakuna mrefu lisilokuwa na mwisho
Hata hili lina mwisho
Majaribu hayana budi kuyavumilia
Nitavumilia oh sitawaza uovu
Manabii walijaribiwa
mitume wengine kufa kwa ajili ya kazi ya Mungu
Nami pia sitavunjika moyo
Vumilia vumilia vumilia jipe moyo
Vumilia vumilia hatimaye utashinda
Vikwazo vingi na vitisho mbele yako
Usiogope usiogope
Ndoa yako japo kiasi hicho
Usiogope jibu lipo leo
Huduma japo pigwa vita hivyo
Usiogope jua yupo mtetezi
Ukimwona nyani mzee
Jua kakwepa mishale mingi
Usiogope yupo mtetezi
Usiogope vita ni vya Bwana
Usiogope vita ni vya Bwana
Sitaogopa sitaogopa
Mungu yuko nami
Sitaogopa sitaogopa
Sitaogopa atanishindia
Sitaogopa sitaogopa
Mungu yuko nami
Sitaogopa sitaogopa
Sitaogopa atanishindia
Jina lako Yesu lina nguvu
Na uweza la kuvunja hila
minyororo ya shetani
Jina lako Yesu lina nguvu
Na uweza la kuvunja hila
minyororo ya shetani
Ulisema Bwana tutatenda
Zaidi ya uliyoyatenda
Naomba Bwana tukiimba
Walio wagonjwa wanapona
Ulisema Bwana tutatenda
Zaidi ya uliyoyatenda
Naomba Bwana tukiimba
Waliopotoka waokoke
Waliokuwa huduma zao zimevunjika
Zinarudi kusimama
Viwete watembee visiwi wasikie ukitajwa
Nguvu za giza zimeshindwa
Ngome za shetani zimeshindwa
Kwa jina lako Kwa jina lako
Jina lako Yesu lina nguvu na uweza
Wa kuvunja hila
minyororo ya shetani
Mauaji ya wake na waume zetu (shindwe)
Chuki kati ya binadamu (shindwe)
Unafiki na masengenyo (shindwe)
In the mighty name of Jesus christ (shindwe)
Every nation bow and every tongue confess
That Jesus is the Lord yeah
Every knee shall bow and every tongue confess
Jesus is the Lord, Jesus the Lord
Jina lako Yesu lina nguvu na uweza
Wa kuvunja hila
minyororo ya shetani
Kila goti lipigwe kila ulimi ukiri
Kwamba wewe ni Bwana, wewe ni Bwana