Chorus / Description :
Na furaha tutaiona,
Mioyo ikitakata sana,
Kwako mwokozi kuonana,
Na milele kukaa.
Twende kwa Yesu, mimi nawe,
Njia atwonya tuijue
Imo chuoni; na mwenyewe,
Hapo asema, njoo!
Na furaha tutaiona,
Mioyo ikitakata sana,
Kwako mwokozi kuonana,
Na milele kukaa.
Wana na waje, ?atwambia.
Furahini mkisikia;
Ndiye mfalme wetu pia,
Na tumtii, njoo.
Na furaha tutaiona,
Mioyo ikitakata sana,
Kwako mwokozi kuonana,
Na milele kukaa.
Wangojeani leo yupo;
Sikiza sana asemapo;
Huruma zake zikwitapo
Ewe kijana njoo
Na furaha tutaiona,
Mioyo ikitakata sana,
Kwako mwokozi kuonana,
Na milele kukaa.