Natasha Lisimo - Asante

Chorus / Description : Wakati wote niwe nawe (Baba)
Machozi yangu yafute (Mungu)
Asante kwa yote (Baba)
Nimekuwa jasiri (Asante)
Asante kwa yote mema
(asante kwa yote)

Asante Lyrics

Ni rahisi moyo lawama linapotokea mbaya 
Ninasahau hayo yote ni mpango wako 
Ninapata shida kichwani ninachanganyikiwa 
Nikumbushe wema wako, wakati wote nikuabudu 
Nikusifu kwa hali zote nisiende mbali nawe 



Wakati wote niwe nawe (Baba) 
Machozi yangu yafute (Mungu)
Wakati wote niwe nawe (Bwana) 
Machozi yangu yafute (Mungu)

Ni wewe ndiwe mfariji wapekee 
Baba wa yatima, mume wa wajane 
Niwezeshe kustahimili kiangazi na masika 
Pepo mbaya na mzuri pale unaponipitia 
Nisimame mbele zako milele milele 
Nishike na mkono wako daima daima 
Maana kila litokalo wewe umepanga litokee 
Sio kwamba nia yako tupotee ila tuzidishe imani 

Wakati wote niwe nawe (Baba) 
Machozi yangu yafute (Mungu)
Wakati wote niwe nawe (Bwana) 
Machozi yangu yafute (Baba) 

Asante kwa yote (Baba) 
Nimekuwa jasiri (Asante) 
Asante kwa yote mema 
(asante kwa yote) 
Kwa utukufu wako (asante) 
Asante Baba (asante) 
Pokea moyo shukurani (asante kwa yote) 
Oh Baba (asante ) 
Nakushukuru kwa njia zako (asante) 
Nakushukuru kwa matendo yako (asante)

Asante Video

  • Song: Asante
  • Artist(s): Natasha Lisimo


Share: