Niko Hapa Baba Niguse Lyrics

By Sifaeli Mwabuka

Lyrics

Najua Baba macho yako yanaona 

Nitazame na mimi 

Najua Baba masikio yako yanasikia 

Sikia maombi yangu 


Ni wengi wamekuona Baba ukijibu 

Jibu na mimi 

Oh ni wengi wamekuona Baba ukitenda 

Tenda kwangu na mimi 


Ni wewe Mungu wangu usiyenaupendeleo 

Niguse na mimi Baba 

Ni wewe Baba usiyenaupendeleo 

Nikumbuke na mimi 


Niko hapa, niko hapa 

Niko hapa Baba uniguse 


Niko hapa, niko hapa 

Niko hapa, Baba uniguse 


Najifunza kwa wengine walionitangulia 

Nafahamu wewe unatenda 

Najifunza kwa Yakobo 

Hakukuacha Baba uende 

Aling'ang'ana na wewe 

Akasema huwezi kwenda usiponibariki 

Yakobo na aseme 

Akasema huwezi kwenda usiponiponya 

Akashika pindo lako yule mwanamke 


Na mimi niko hapa 

Niko hapa, niko hapa 

Niko hapa Baba uniponye  

Niko hapa, niko hapa 

Niko hapa Baba uniguse  


Niko hapa, niko hapa 

Niko hapa, Baba uniguse 


NIKO HAPA BABA NIGUSE BY SIFAELI MWABUKA. SKIZA 5708290

Now Playing...