Sio Bure

By Zabron Singers

Lyrics

Sio si bure eeh wala si utani 

Sio utani twaendelea 

Tujeshi kubwa safarini pamoja 

Njiani moja mpaka Jerusalemu 


Safari yetu kamwe si bure 

Tuna hakika na uzima uzima 

Maana tuwazao wa wauteule 

Tumefanyika wana wa Mungu 

Miliki safi tena ndani ya Yesu 

Kusali kwetu kwa hakika si bure 


Sio sio si bure kwa Yesu ni faida 

Tuna sehemu ya kupeleka shida 

Wema nazo fadhili zake zimetukuka 

Toka toka juu kule Mungu hutazama 

Aone kama kuna wamtafutao 

Tafutane Mungu maana apatikana 

Ukipata Mungu umepata uzima 


Hatukatai kweli kuna vikwazo 

Vitisho vingi kukatisha tamaa 

Hatuogopi maana tuko na Yesu 

Kusimamia safari yetu 

Hakuna jambo gumu la kumshinda 

Iwe ni kifo tena kwake ni mwisho 

Mwisho wa yote ntaishi naye  

Hapo ndio mwisho wa safari yetu 

Maumivu kwisha habari yake 


Sio sio si bure kwa Yesu ni faida 

Tuna sehemu ya kupeleka shida 

Wema nazo fadhili zake zimetukuka 

Toka toka juu kule Mungu hutazama 

Aone kama kuna wamtafutao 

Tafutane Mungu maana apatikana 

Ukipata Mungu umepata uzima