Imenigharimu

By Zabron Singers

Lyrics

Imenigharimu sana mimi kuwa hapa 

Wacha Mungu awe Mungu 

Tangu kuzaliwa kwangu ujana uzee 

Hajawai mi niacha 


Kwenye giza kaniwekea nuru nisihangaike 

Kwenye shida hutengeneza njia watu wake tunapita

Nimekuja kugundua umbali umenileta 

Acha Mungu nikusifu 


Mimi sina Mungu mwingine wa kunitendea haya 

Hakika wanikumbuka 

Hivi nilivyo Mungu ni yeye kaniwezesha 

Ni muweza Baba heehee

Ntaendela kuvuka popote niko na Mungu 

Ni Mungu yuko na mimi 


Ni mengi nimepitia na leo kufika hapa 

Kama si Mungu ni nani? Wadhani nani tena 

Mengi akanivusha na baraka zikapanda 

Wadhani Mungu ni nani, ni nani


Yeye ni nani, wadhani ni nani 

Mungu ni nani eeh eeh


Kuzihesabu tu siku ni nguvu za Mungu 

Ndio maana niko hai 

Sikumlipa chochote, 

wakati wa Mungu unapofika umefika 


Nilipokuita hukusita, ulisema nami 

Ninakushukuru umenipa maisha mazuri  


Nimekuja kugundua wewe ni Mungu mwenye nguvu 

Mwenye mamlaka yote 

Sababu niko na wewe sina hofu na mashaka 

Vita si yangu ni yako 


Hivi nilivyo Mungu ni yeye kaniwezesha 

Ni muweza Baba heehee

Ntaendela kuvuka popote niko na Mungu 

Ni Mungu yuko na mimi 


Ni mengi nimepitia na leo kufika hapa 

Kama si Mungu ni nani? Wadhani nani tena 

Mengi akanivusha na baraka zikapanda 

Wadhani Mungu ni nani, ni nani


Utabaki kuwa Mungu uu

Imenigharimu by zabron singers