Sweetie Sweetie

By Zabron Singers

Lyrics

Hatimaye ni leo ni siku yetu 

Siku yetu muhimu harusi yetu 

Kuwepo kwenyu kwetu muhimu 

Kwetu nyinyi ni ndugu leo na kesho 


Harusi maua ng'ari ng'ari wanapendeza 

Leo ni furaha shangwe na furaha 

Harusi maua tabasamu, suti na shela 

Wacha tufurahi sote tufurahi 


Sweetie sweetie sweetie 

Haikuwa rahisi tufike leo hii 

Na hapa tulipo ndio siku yetu 

Ipo ukivu ya harusi 


Sasa nyumba moja mwili mmoja 

Kila kitu ni moja tuwe pamoja 

Upendo naongeza nawe ongeza 

Heshima napandisha tuwe pamoja 


Sweetie sweetie sweetie 

Haikuwa rahisi tufike leo hii 

Na hapa tulipo ndio siku yetu 

Ipo ukivu ya harusi 


Sasa wewe ni mimi, mimi ni wewe 

Wewe ndio wendani wangu rafiki yangu 


Na wazazi wameona wakaturusu 

Kwa furaha wakasema tumewabariki 

Na mwenyezi maulana atatubariki 

Tukazae na tulee watoto wazuri 


Sweetie sweetie sweetie 

Haikuwa rahisi tufike leo hii 

Na hapa tulipo ndio siku yetu 

Ipo ukivu ya harusi 


Sasa nyumba moja mwili mmoja 

Kila kitu ni moja tuwe pamoja 

Upendo naongeza nawe ongeza 

Heshima napandisha tuwe pamoja 


Sweetie sweetie sweetie 

Haikuwa rahisi tufike leo hii (my love)

Na hapa tulipo ndio siku yetu 

Ipo ukivu ya harusi 


Ya ndoa mengi mengi tupande nayo 

Sweetie nikuheshimu uniheshimu 

Mahaba moto moto yawe ni wimbo 

KWetu yakawe waridi yakanukie 


Walikuweko nao walitamani 

Wakaparangana haikuwezekana 

Nasi Mungu tusingefika hapa na kufurahi hivi 

Leo ni leo mambo sasa ni mambo


Sweetie sweetie sweetie 

Haikuwa rahisi tufike leo hii (my baby)

Na hapa tulipo ndio siku yetu 

Ipo ukivu ya harusi 


Sasa nyumba moja mwili mmoja 

Kila kitu ni moja tuwe pamoja 

Upendo naongeza nawe ongeza 

Heshima napandisha tuwe pamoja 


Na tutakumbushana kukaa na Mungu 

Familia ya Mungu hujaa upendo 

Wema kwa ndugu zote wa pande zote 

Tutapendwa na wote hata na Mungu 

ZABRON SINGERS- SWEETIE SWEETIE! (SMS SKIZA 7639929 TO 811)