Usiniache

By Zabron Singers

Lyrics

Sitaki kuwa wa hivi hivi mimi 

Kuipenda dunia nikaikosa mbingu 

Kuwa vumbi la jibu kwa watakatifu 

Litakalo kanyagwa na washindi wa dhambi


Duniani mbingu tuwe wote 

Mbali ulikonitoa usiniache 

Ikiwa umeniheshimisha hapa chini 

Yesu akija ruhusu niende na yeye 


Ninafurahi kuona vile unanijali 

Nikiwa mdogo mkubwa uko na mimi 

Kwenye vikwazo vitisho umekuwa na mimi 

Mchana usiku bega kwa bega uko na mimi 


(Usiniache Mungu wangu) Baba 

Baba tangu ni mdogo mdogo 

Umekuwa nami siku zote 

(Umenibariki na vingi ukanisamehe mengi)

Baba ukinibariki nikumbushe nisikusahau 

(Nia yangu unimiliki Baba)

Baba unapo mpango pale Yerusalemu 

(Jana leo hata kesho)

unikumbuke niwe pale 

(Usiniache Mungu wangu) Baba 

(Usiniache Mungu wangu) Baba 

Siku zote


Lutu alikata kubaki hivyo hivyo 

Kakataa kupenda uovu wa Sodoma 

Katikati ya mji wa uovu wa dhambi 

Kwa uaminifu akamuakilisha Mungu 


Naomba nami niwe mtumwa mwaminifu 

Niwakilishe vyema jina la Yesu 

Hata kama dunia ikithiri uovu 

Ruhusu nisimame nikutetee


Na siku ile mwokozi wangu atakaporudi 

Aseme vyema wewe ni mtumishi mwema 

Kisha nipae nipae mawinguni na Yesu 

Kuanzisha familia mpya na Mungu 


(Usiniache Mungu wangu) Baba 

Baba tangu ni mdogo mdogo 

Umekuwa nami siku zote 

(Umenibariki na vingi ukanisamehe mengi)

Baba ukinibariki nikumbushe nisikusahau 

(Nia yangu unimiliki Baba)

Baba unapo mpango pale Yerusalemu 

(Jana leo hata kesho)

unikumbuke niwe pale 

(Usiniache Mungu wangu) Baba 

(Usiniache Mungu wangu) Baba 

Siku zote

USINIACHE BY ZABRON SINGERS (SMS SKIZA 5961248 TO 811)