1 Wathesalonike Mlango 1 1st Thessalonians
1 Wathesalonike 1:1 1stThessalonians 1:1
Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani.
1 Wathesalonike 1:2 1stThessalonians 1:2
Twamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu nyote, tukiwataja katika maombi yetu.
1 Wathesalonike 1:3 1stThessalonians 1:3
Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na saburi yenu ya tumaini lililo katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu.
1 Wathesalonike 1:4 1stThessalonians 1:4
Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu;
1 Wathesalonike 1:5 1stThessalonians 1:5
ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; kama vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu.
1 Wathesalonike 1:6 1stThessalonians 1:6
Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu.
1 Wathesalonike 1:7 1stThessalonians 1:7
Hata mkawa kielelezo kwa watu wote waaminio katika Makedonia, na katika Akaya.
1 Wathesalonike 1:8 1stThessalonians 1:8
Maana kutoka kwenu neno la Mungu limevuma, si katika Makedonia na Akaya tu, ila na kila mahali imani yenu mliyo nayo kwa Mungu imeenea; hata hatuna haja sisi kunena lo lote.
1 Wathesalonike 1:9 1stThessalonians 1:9
Kwa kuwa wao wenyewe wanatangaza habari zetu, jinsi kulivyokuwa kuingia kwetu kwenu; na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaziacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai, wa kweli;
1 Wathesalonike 1:10 1stThessalonians 1:10
na kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni Yesu, mwenye kutuokoa na ghadhabu itakayokuja.