1 Wathesalonike Mlango 5 1st Thessalonians
1 Wathesalonike 5:1 1stThessalonians 5:1
Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
1 Wathesalonike 5:2 1stThessalonians 5:2
Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
1 Wathesalonike 5:3 1stThessalonians 5:3
Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
1 Wathesalonike 5:4 1stThessalonians 5:4
Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.
1 Wathesalonike 5:5 1stThessalonians 5:5
Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
1 Wathesalonike 5:6 1stThessalonians 5:6
Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
1 Wathesalonike 5:7 1stThessalonians 5:7
Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.
1 Wathesalonike 5:8 1stThessalonians 5:8
Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
1 Wathesalonike 5:9 1stThessalonians 5:9
Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
1 Wathesalonike 5:10 1stThessalonians 5:10
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.
1 Wathesalonike 5:11 1stThessalonians 5:11
Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.
1 Wathesalonike 5:12 1stThessalonians 5:12
Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;
1 Wathesalonike 5:13 1stThessalonians 5:13
mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.
1 Wathesalonike 5:14 1stThessalonians 5:14
Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.
1 Wathesalonike 5:15 1stThessalonians 5:15
Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
1 Wathesalonike 5:16 1stThessalonians 5:16
Furahini siku zote;
1 Wathesalonike 5:17 1stThessalonians 5:17
ombeni bila kukoma;
1 Wathesalonike 5:18 1stThessalonians 5:18
shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.
1 Wathesalonike 5:19 1stThessalonians 5:19
Msimzimishe Roho;
1 Wathesalonike 5:20 1stThessalonians 5:20
msitweze unabii;
1 Wathesalonike 5:21 1stThessalonians 5:21
jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;
1 Wathesalonike 5:22 1stThessalonians 5:22
jitengeni na ubaya wa kila namna.
1 Wathesalonike 5:23 1stThessalonians 5:23
Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Wathesalonike 5:24 1stThessalonians 5:24
Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.
1 Wathesalonike 5:25 1stThessalonians 5:25
Ndugu, tuombeeni.
1 Wathesalonike 5:26 1stThessalonians 5:26
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
1 Wathesalonike 5:27 1stThessalonians 5:27
Nawaapisha kwa Bwana, ndugu wote wasomewe waraka huu.
1 Wathesalonike 5:28 1stThessalonians 5:28
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.