1 Wathesalonike Mlango 5 1st Thessalonians

1 Wathesalonike 5:1 1stThessalonians 5:1

Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

1 Wathesalonike 5:2 1stThessalonians 5:2

Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

1 Wathesalonike 5:3 1stThessalonians 5:3

Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

1 Wathesalonike 5:4 1stThessalonians 5:4

Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

1 Wathesalonike 5:5 1stThessalonians 5:5

Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

1 Wathesalonike 5:6 1stThessalonians 5:6

Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

1 Wathesalonike 5:7 1stThessalonians 5:7

Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.

1 Wathesalonike 5:8 1stThessalonians 5:8

Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

1 Wathesalonike 5:9 1stThessalonians 5:9

Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;

1 Wathesalonike 5:10 1stThessalonians 5:10

ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.

1 Wathesalonike 5:11 1stThessalonians 5:11

Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.

1 Wathesalonike 5:12 1stThessalonians 5:12

Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;

1 Wathesalonike 5:13 1stThessalonians 5:13

mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

1 Wathesalonike 5:14 1stThessalonians 5:14

Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.

1 Wathesalonike 5:15 1stThessalonians 5:15

Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.

1 Wathesalonike 5:18 1stThessalonians 5:18

shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.

1 Wathesalonike 5:21 1stThessalonians 5:21

jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;

1 Wathesalonike 5:22 1stThessalonians 5:22

jitengeni na ubaya wa kila namna.

1 Wathesalonike 5:23 1stThessalonians 5:23

Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

1 Wathesalonike 5:24 1stThessalonians 5:24

Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.

1 Wathesalonike 5:26 1stThessalonians 5:26

Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.

1 Wathesalonike 5:27 1stThessalonians 5:27

Nawaapisha kwa Bwana, ndugu wote wasomewe waraka huu.

1 Wathesalonike 5:28 1stThessalonians 5:28

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.