1 Wathesalonike Mlango 3 1st Thessalonians

1 Wathesalonike 3:1 1stThessalonians 3:1

Basi kwa hiyo, tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliona vema kuachwa Athene peke yetu.

1 Wathesalonike 3:2 1stThessalonians 3:2

Tukamtuma Timotheo ndugu yetu, mtumishi wa Mungu katika Injili ya Kristo, ili kuwafanya ninyi imara na kuwafariji kwa habari ya imani yenu;

1 Wathesalonike 3:3 1stThessalonians 3:3

mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.

1 Wathesalonike 3:4 1stThessalonians 3:4

Kwa kuwa tulipokuwapo kwenu tulitangulia kuwaambia kwamba tutapata dhiki, kama ilivyotukia, nanyi mwajua.

1 Wathesalonike 3:5 1stThessalonians 3:5

Kwa hiyo mimi nami nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nalituma mtu ili niijue imani yenu, asije yule mjaribu akawajaribu, na taabu yetu ikawa haina faida.

1 Wathesalonike 3:6 1stThessalonians 3:6

Lakini Timotheo alipotujia hivi sasa kutoka kwenu, alituletea habari njema za imani yenu na upendo wenu, na ya kwamba mnatukumbuka vema siku zote; mkitamani kutuona sisi vile vile kama sisi kuwaona ninyi.

1 Wathesalonike 3:7 1stThessalonians 3:7

Kwa sababu hiyo, ndugu, tulifarijiwa kwa habari zenu, katika msiba na dhiki yetu yote, kwa imani yenu.

1 Wathesalonike 3:8 1stThessalonians 3:8

Kwa kuwa sasa twaishi, ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana.

1 Wathesalonike 3:9 1stThessalonians 3:9

Maana ni shukrani gani tuwezayo kumlipa Mungu kwa ajili yenu, kwa furaha ile yote tunayoifurahia, kwa sababu yenu mbele za Mungu wetu;

1 Wathesalonike 3:10 1stThessalonians 3:10

usiku na mchana tunapoomba kwa juhudi tupate kuwaona nyuso zenu, na kuyatengeneza mapungufu ya imani yenu?

1 Wathesalonike 3:11 1stThessalonians 3:11

Basi Mungu mwenyewe, Baba yetu, na Bwana wetu Yesu, atuongoze njia yetu tufike kwenu.

1 Wathesalonike 3:12 1stThessalonians 3:12

Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

1 Wathesalonike 3:13 1stThessalonians 3:13

apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.