1 Wathesalonike Mlango 3 1st Thessalonians
1 Wathesalonike 3:1 1stThessalonians 3:1
Basi kwa hiyo, tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliona vema kuachwa Athene peke yetu.
1 Wathesalonike 3:2 1stThessalonians 3:2
Tukamtuma Timotheo ndugu yetu, mtumishi wa Mungu katika Injili ya Kristo, ili kuwafanya ninyi imara na kuwafariji kwa habari ya imani yenu;
1 Wathesalonike 3:3 1stThessalonians 3:3
mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
1 Wathesalonike 3:4 1stThessalonians 3:4
Kwa kuwa tulipokuwapo kwenu tulitangulia kuwaambia kwamba tutapata dhiki, kama ilivyotukia, nanyi mwajua.
1 Wathesalonike 3:5 1stThessalonians 3:5
Kwa hiyo mimi nami nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nalituma mtu ili niijue imani yenu, asije yule mjaribu akawajaribu, na taabu yetu ikawa haina faida.
1 Wathesalonike 3:6 1stThessalonians 3:6
Lakini Timotheo alipotujia hivi sasa kutoka kwenu, alituletea habari njema za imani yenu na upendo wenu, na ya kwamba mnatukumbuka vema siku zote; mkitamani kutuona sisi vile vile kama sisi kuwaona ninyi.
1 Wathesalonike 3:7 1stThessalonians 3:7
Kwa sababu hiyo, ndugu, tulifarijiwa kwa habari zenu, katika msiba na dhiki yetu yote, kwa imani yenu.
1 Wathesalonike 3:8 1stThessalonians 3:8
Kwa kuwa sasa twaishi, ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana.
1 Wathesalonike 3:9 1stThessalonians 3:9
Maana ni shukrani gani tuwezayo kumlipa Mungu kwa ajili yenu, kwa furaha ile yote tunayoifurahia, kwa sababu yenu mbele za Mungu wetu;
1 Wathesalonike 3:10 1stThessalonians 3:10
usiku na mchana tunapoomba kwa juhudi tupate kuwaona nyuso zenu, na kuyatengeneza mapungufu ya imani yenu?
1 Wathesalonike 3:11 1stThessalonians 3:11
Basi Mungu mwenyewe, Baba yetu, na Bwana wetu Yesu, atuongoze njia yetu tufike kwenu.
1 Wathesalonike 3:12 1stThessalonians 3:12
Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;
1 Wathesalonike 3:13 1stThessalonians 3:13
apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.