1 Wathesalonike Mlango 4 1st Thessalonians
1 Wathesalonike 4:1 1stThessalonians 4:1
Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana.
1 Wathesalonike 4:2 1stThessalonians 4:2
Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.
1 Wathesalonike 4:3 1stThessalonians 4:3
Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;
1 Wathesalonike 4:4 1stThessalonians 4:4
kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;
1 Wathesalonike 4:5 1stThessalonians 4:5
si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.
1 Wathesalonike 4:6 1stThessalonians 4:6
Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosa katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.
1 Wathesalonike 4:7 1stThessalonians 4:7
Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.
1 Wathesalonike 4:8 1stThessalonians 4:8
Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
1 Wathesalonike 4:9 1stThessalonians 4:9
Katika habari ya upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.
1 Wathesalonike 4:10 1stThessalonians 4:10
Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini twawasihi, ndugu, mzidi sana.
1 Wathesalonike 4:11 1stThessalonians 4:11
Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;
1 Wathesalonike 4:12 1stThessalonians 4:12
ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote.
1 Wathesalonike 4:13 1stThessalonians 4:13
Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
1 Wathesalonike 4:14 1stThessalonians 4:14
Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
1 Wathesalonike 4:15 1stThessalonians 4:15
Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
1 Wathesalonike 4:16 1stThessalonians 4:16
Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
1 Wathesalonike 4:17 1stThessalonians 4:17
Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
1 Wathesalonike 4:18 1stThessalonians 4:18
Basi, farijianeni kwa maneno hayo.