1 Wathesalonike Mlango 4 1st Thessalonians

1 Wathesalonike 4:1 1stThessalonians 4:1

Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana.

1 Wathesalonike 4:2 1stThessalonians 4:2

Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.

1 Wathesalonike 4:3 1stThessalonians 4:3

Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

1 Wathesalonike 4:4 1stThessalonians 4:4

kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

1 Wathesalonike 4:5 1stThessalonians 4:5

si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.

1 Wathesalonike 4:6 1stThessalonians 4:6

Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosa katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.

1 Wathesalonike 4:7 1stThessalonians 4:7

Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.

1 Wathesalonike 4:8 1stThessalonians 4:8

Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.

1 Wathesalonike 4:9 1stThessalonians 4:9

Katika habari ya upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.

1 Wathesalonike 4:10 1stThessalonians 4:10

Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini twawasihi, ndugu, mzidi sana.

1 Wathesalonike 4:11 1stThessalonians 4:11

Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;

1 Wathesalonike 4:12 1stThessalonians 4:12

ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote.

1 Wathesalonike 4:13 1stThessalonians 4:13

Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

1 Wathesalonike 4:14 1stThessalonians 4:14

Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.

1 Wathesalonike 4:15 1stThessalonians 4:15

Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

1 Wathesalonike 4:16 1stThessalonians 4:16

Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

1 Wathesalonike 4:17 1stThessalonians 4:17

Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

1 Wathesalonike 4:18 1stThessalonians 4:18

Basi, farijianeni kwa maneno hayo.