Zabron Singers - Usiniache

Chorus / Description : (Usiniache Mungu wangu) Baba
Baba tangu ni mdogo mdogo
Umekuwa nami siku zote
(Umenibariki na vingi ukanisamehe mengi)
Baba ukinibariki nikumbushe nisikusahau
(Nia yangu unimiliki Baba)
Baba unapo mpango pale Yerusalemu
(Jana leo hata kesho)
unikumbuke niwe pale
(Usiniache Mungu wangu) Baba
(Usiniache Mungu wangu) Baba
Siku zote

Usiniache Lyrics

Sitaki kuwa wa hivi hivi mimi 
Kuipenda dunia nikaikosa mbingu 
Kuwa vumbi la jibu kwa watakatifu 
Litakalo kanyagwa na washindi wa dhambi

Duniani mbingu tuwe wote 
Mbali ulikonitoa usiniache 
Ikiwa umeniheshimisha hapa chini 
Yesu akija ruhusu niende na yeye 

Ninafurahi kuona vile unanijali 
Nikiwa mdogo mkubwa uko na mimi 
Kwenye vikwazo vitisho umekuwa na mimi 
Mchana usiku bega kwa bega uko na mimi 

(Usiniache Mungu wangu) Baba 
Baba tangu ni mdogo mdogo 
Umekuwa nami siku zote 
(Umenibariki na vingi ukanisamehe mengi)
Baba ukinibariki nikumbushe nisikusahau 
(Nia yangu unimiliki Baba)
Baba unapo mpango pale Yerusalemu 
(Jana leo hata kesho)
unikumbuke niwe pale 
(Usiniache Mungu wangu) Baba 
(Usiniache Mungu wangu) Baba 
Siku zote

Lutu alikata kubaki hivyo hivyo 
Kakataa kupenda uovu wa Sodoma 
Katikati ya mji wa uovu wa dhambi 
Kwa uaminifu akamuakilisha Mungu 

Naomba nami niwe mtumwa mwaminifu 
Niwakilishe vyema jina la Yesu 
Hata kama dunia ikithiri uovu 
Ruhusu nisimame nikutetee

Na siku ile mwokozi wangu atakaporudi 
Aseme vyema wewe ni mtumishi mwema 
Kisha nipae nipae mawinguni na Yesu 
Kuanzisha familia mpya na Mungu 

(Usiniache Mungu wangu) Baba 
Baba tangu ni mdogo mdogo 
Umekuwa nami siku zote 
(Umenibariki na vingi ukanisamehe mengi)
Baba ukinibariki nikumbushe nisikusahau 
(Nia yangu unimiliki Baba)
Baba unapo mpango pale Yerusalemu 
(Jana leo hata kesho)
unikumbuke niwe pale 
(Usiniache Mungu wangu) Baba 
(Usiniache Mungu wangu) Baba 
Siku zote

Usiniache Video

  • Song: Usiniache
  • Artist(s): Zabron Singers


Share: