1 Timotheo Mlango 5 1st Timothy

1 Timotheo 5:1 1stTimothy 5:1

Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;

1 Timotheo 5:2 1stTimothy 5:2

wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote.

1 Timotheo 5:3 1stTimothy 5:3

Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli.

1 Timotheo 5:4 1stTimothy 5:4

Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.

1 Timotheo 5:5 1stTimothy 5:5

Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku.

1 Timotheo 5:6 1stTimothy 5:6

Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.

1 Timotheo 5:7 1stTimothy 5:7

Mambo hayo pia uyaagize, ili wasiwe na lawama.

1 Timotheo 5:8 1stTimothy 5:8

Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

1 Timotheo 5:9 1stTimothy 5:9

Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja;

1 Timotheo 5:10 1stTimothy 5:10

naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema.

1 Timotheo 5:11 1stTimothy 5:11

Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;

1 Timotheo 5:12 1stTimothy 5:12

nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza.

1 Timotheo 5:13 1stTimothy 5:13

Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.

1 Timotheo 5:14 1stTimothy 5:14

Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu.

1 Timotheo 5:15 1stTimothy 5:15

Kwa maana wengine wamekwisha kugeuka na kumfuata Shetani.

1 Timotheo 5:16 1stTimothy 5:16

Mwanamke aaminiye, akiwa ana wajane, na awasaidie mwenyewe, Kanisa lisilemewe; ili liwasaidie wale walio wajane kweli kweli.

1 Timotheo 5:17 1stTimothy 5:17

Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.

1 Timotheo 5:18 1stTimothy 5:18

Kwa maana andiko lasema, Usimfunge kinywa ng'ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake.

1 Timotheo 5:19 1stTimothy 5:19

Usikubali mashitaka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.

1 Timotheo 5:20 1stTimothy 5:20

Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.

1 Timotheo 5:21 1stTimothy 5:21

Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, na mbele za malaika wateule, uyatende hayo pasipo kuhukumu kwa haraka; usifanye neno lo lote kwa upendeleo.

1 Timotheo 5:22 1stTimothy 5:22

Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi.

1 Timotheo 5:23 1stTimothy 5:23

Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara.

1 Timotheo 5:24 1stTimothy 5:24

Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata.

1 Timotheo 5:25 1stTimothy 5:25

Vivyo hivyo matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi kusitirika.