1 Timotheo Mlango 6 1st Timothy

1 Timotheo 6:1 1stTimothy 6:1

Wo wote walio chini ya kongwa, hali ya utumwa, na wawahesabie bwana zao kuwa wamestahili heshima yote, jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu.

1 Timotheo 6:2 1stTimothy 6:2

Na wale walio na bwana waaminio wasiwadharau kwa kuwa ni ndugu; bali afadhali wawatumikie, kwa sababu hao waishirikio faida ya kazi yao wamekuwa wenye imani na kupendwa. Mambo hayo uyafundishe na kuonya.

1 Timotheo 6:3 1stTimothy 6:3

Mtu awaye yote akifundisha elimu nyingine, wala hayakubali maneno yenye uzima ya Bwana wetu Yesu Kristo, wala mafundisho yapatanayo na utauwa,

1 Timotheo 6:4 1stTimothy 6:4

amejivuna; wala hafahamu neno lo lote; bali ana wazimu wa kuwazia habari za maswali, na mashindano ya maneno, ambayo katika hayo hutoka husuda, na ugomvi, na matukano, na shuku mbaya;

1 Timotheo 6:5 1stTimothy 6:5

na majadiliano ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida.

1 Timotheo 6:6 1stTimothy 6:6

Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.

1 Timotheo 6:7 1stTimothy 6:7

Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu;

1 Timotheo 6:8 1stTimothy 6:8

ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.

1 Timotheo 6:9 1stTimothy 6:9

Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.

1 Timotheo 6:10 1stTimothy 6:10

Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.

1 Timotheo 6:11 1stTimothy 6:11

Bali wewe, mtu wa Mungu, uyakimbie mambo hayo; ukafuate haki, utauwa, imani, upendo, saburi, upole.

1 Timotheo 6:12 1stTimothy 6:12

Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi.

1 Timotheo 6:13 1stTimothy 6:13

Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato,

1 Timotheo 6:14 1stTimothy 6:14

kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo;

1 Timotheo 6:15 1stTimothy 6:15

ambako yeye kwa majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana;

1 Timotheo 6:16 1stTimothy 6:16

ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.

1 Timotheo 6:17 1stTimothy 6:17

Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha.

1 Timotheo 6:18 1stTimothy 6:18

Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo;

1 Timotheo 6:19 1stTimothy 6:19

huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli.

1 Timotheo 6:20 1stTimothy 6:20

Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo;

1 Timotheo 6:21 1stTimothy 6:21

ambayo wengine wakiikiri hiyo wameikosa Imani. Neema na iwe pamoja nanyi.