Yoshua Mlango 12 Joshua

Yoshua 12:1 Joshua 12:1

Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao wana wa Israeli waliwapiga na kuimiliki nchi yao ng'ambo ya pili ya Yordani, upande wa maawio ya jua, kutoka bonde la Amoni mpaka mlima wa Hermoni, na nchi yote ya Araba upande wa mashariki;

Yoshua 12:2 Joshua 12:2

Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekaa huko Heshboni, naye ndiye aliyetawala toka Aroeri, ulioko kando ya bonde la Arnoni, na toka huo mji ulio katikati ya bonde, na nusu ya Gileadi, hata kuufikilia mto wa Yaboki, mpaka wa hao wana wa Amoni;

Yoshua 12:3 Joshua 12:3

na nchi ya Araba mpaka bahari ya Kinerethi, kuelekea mashariki, tena mpaka bahari ya Ataba, mpaka Bahari ya Chumvi, kwendea mashariki, njia ya kwendea Beth-yeshimothi; tena upande wa kusini, chini ya matelemko ya Pisga;

Yoshua 12:4 Joshua 12:4

tena mpaka wa Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa wa hayo mabaki ya hao Warefai, aliyekaa Ashtarothi na Edrei,

Yoshua 12:5 Joshua 12:5

naye alitawala katika mlima wa Hermoni, na katika Saleka, na katika Bashani yote, hata mpaka wa Wageshuri, na Wamaaka, na nusu ya Gileadi, mpaka wa huyo Sihoni mfalme wa Heshboni.

Yoshua 12:6 Joshua 12:6

Musa mtumishi wa Bwana na wana wa Israeli wakawapiga; naye Musa mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, na Wagadi, na nusu ya kabila ya Manase iwe urithi wao.

Yoshua 12:7 Joshua 12:7

Hawa ni wafalme wa hiyo nchi ambao Yoshua na wana wa Israeli waliwapiga ng'ambo ya pili ya Yordani upande wa magharibi, kutoka Baal-gadi katika bonde la Lebanoni mpaka kilima cha Halaki, kilichoelekea Seiri; Yoshua naye akawapa kabila za Israeli iwe milki yao sawasawa na magawanyo yao;

Yoshua 12:8 Joshua 12:8

katika nchi ya vilima, na katika Shefela, na katika nchi ya Araba, na katika matelemko, na katika bara, na katika Negebu; nchi ya Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi;

Yoshua 12:9 Joshua 12:9

mfalme wa Yeriko, mmoja; mfalme wa Ai, ulio karibu na Betheli, mmoja;

Yoshua 12:10 Joshua 12:10

mfalme wa Yerusalemu, mmoja; mfalme wa Hebroni, mmoja;

Yoshua 12:11 Joshua 12:11

mfalme wa Yarmuthi, mmoja; na mfalme wa Lakishi, mmoja;

Yoshua 12:12 Joshua 12:12

mfalme wa Egloni, mmoja; na mfalme wa Gezeri, mmoja;

Yoshua 12:13 Joshua 12:13

mfalme wa Debiri, mmoja; na mfalme wa Gederi, mmoja;

Yoshua 12:14 Joshua 12:14

mfalme wa Horma, mmoja; na mfalme wa Aradi, mmoja;

Yoshua 12:15 Joshua 12:15

mfalme wa Libna, mmoja; na mfalme wa Adulamu, mmoja;

Yoshua 12:16 Joshua 12:16

mfalme wa Makeda, mmoja; na mfalme wa Betheli, mmoja;

Yoshua 12:17 Joshua 12:17

mfalme wa Tapua, mmoja; na mfalme wa Heferi, mmoja;

Yoshua 12:18 Joshua 12:18

mfalme wa Afeka, mmoja; na mfalme wa Lasharoni, mmoja;

Yoshua 12:19 Joshua 12:19

mfalme wa Madoni, mmoja; na mfalme wa Hazori, mmoja;

Yoshua 12:20 Joshua 12:20

mfalme wa Shimron-meroni, mmoja; na mfalme wa Akshafu, mmoja;

Yoshua 12:21 Joshua 12:21

mfalme wa Taanaki, mmoja; na mfalme wa Megido, mmoja;

Yoshua 12:22 Joshua 12:22

na mfalme wa Kedeshi, mmoja; mfalme wa Yokneamu wa Karmeli, mmoja;

Yoshua 12:23 Joshua 12:23

mfalme wa Dori katika kilima cha Dori, mmoja; na mfalme wa makabila katika Gilgali, mmoja;

Yoshua 12:24 Joshua 12:24

na mfalme wa Tirsa, mmoja; wafalme hao wote walikuwa ni thelathini na mmoja.