Mateso

By Erick Smith

Lyrics

Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 

Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 


Nikikumbuka mateso yake Yesu 

Alivyoteseka pale msalabani.

Fimbo, misumari, taji ya miba 

Mkuki ubavuni na kutemewa mate. 


Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 

Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 

Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki 

(rudia) 


Wakamkamata Yesu kama mwizi 

Na kumdharau Yesu mwana wa Mungu. 

Wakamkamata kama mwizi 

Wakumdharau Bwana mwana wa Mungu. 

Wakadhani kuwa ndio mwisho 

Kumbe ndio mwanzo wa wokovu wangu 

Kumbe ndio mwanzo wa wokovu wetu. 


Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 

Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 

Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki 

(rudia) 


Akasulubiwa Yesu Ju ya msalaba 

Akasema Baba, Baba oh wasamehe 

Kwani hawajui walitendalo oh ooh 

Ndipo Bwana wangu akakata roho 

Ndipo Bwana wangu akakata roho  


Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 

Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 


Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 

Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 

Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki

Erick Smith - Mateso (Official Video)