Mifulizo Ya Baraka Lyrics

By The Saints Ministers

Lyrics

Mungu, Elshadai wetu, matendo yako makuu, 

umetukamilisha twajivunia (mifulizo) ya baraka zako.


Twala, twanywa, twalala, twaamka, 

uaminifu wako kwetu mkuu, 

Hitaji letu tunalo 

baraka zako zafululiza twashukuru kwazo.


1. Hannah alibezwa kwa kukosa mtoto, 

hakukataa tamaa, aliomba, wakati wa Mungu ulipofika 

Samweli kazaliwa baraka nyumbani mwake.


2. Waangalieni Ndege wa angani, hawapandi wala hawavuni, 

hawakusanyi ghalani, ila Baba wa mbinguni huwalisha hao.


Twala, twanywa, twalala, twaamka, uaminifu wako kwetu mkuu, 

Hitaji letu tunalo baraka zako zafululiza twashukuru kwazo.


Wengine walala hoi nawe wala na kusaaza wahitaji nini? 

Mbona walilia cheo wengine hawana kazi, wahitaji nini? 

Wengine wamelazwa na wewe una afya.. Mshukuru Mungu..


Hesabu mibaraka moja moja, aogeleavyo papa baharini,  

Mwanga wa jua hung'aa kote mvua ya masika hutunyea ilivyo baraka zake. 


Ilivyo nyota angani ndivyo baraka zake, Utukuzwe Mungu. 


Mungu, Elshadai wetu, matendo yako makuu, 

umetukamilisha twajivunia (mifulizo) ya baraka

Now Playing...