Watangoja Sana Lyrics

By Annastacia Mukabwa

Lyrics

watangoja sana 

Wanaongoja kuanguka kwako 

Wanaongoja kushindwa kwako 

Wanaongoja umuache Yesu 

Wanaongoja uharibikiwe wacheke 


Waambie pole, pole pole 

Ninaye Yesu, ninaye mwokozi 

Waambie pole, pole pole 

Watangoja sana 


Yesu alipokufa akazikwa kaburini 

Wengi walicheka sana Wengine walisema 

“Si unajifanya ni mwana wa Mungu” 

“Hebu jifufue tukuone” 

Waliweka na walinzi walinde kaburi 

Ili Yesu asifufuke 

Waliweka na jiwe kubwa, pale kaburini 

Ili Yesu asifufuke, Siku ya tatu ilipofika 

Walinzi walishangaa, Yesu hayupo kaburini 

Siku ya tatu ilipofika, Walinzi walishangaa 

Yesu hayupo kaburini, amefufuka 


watangoja sana 

Wanaongoja matanga yako,

Wanaongoja urudiwe kwenyu nani wateleza 

Wanaongoja ufutwe kazi wacheke 


Waambie, pole, pole, pole 

Ninaye yesu sibabaiki mimi nalindwa na Jehova 

Ananipigia vita, Watangoja sana


Eh ni Mungu pekee yake

Analalamishwa juu yako 

Hakuna silaha itainuka 

Kinyume chako ifanikiwe

Maneno ya watu yasikuvunje moyo 

Tegemea we utashinda, utashinda 


watangoja sana 

Wanaongoja kuanguka kwako 

Wanaotaka ndoa yako ivunjike wacheke 

Wanaotamani ufilisike wacheke 

Wanaosema utakufa bila kuzaa mama 


Waambie pole, pole, pole 

Ninalindwa na jeshi la mbinguni 

Wambie, pole, pole, pole 

Watangoja sana 


watangoja sana, Wanasema hutaolewa 

Wanasema utashindwa na elimu 

Wanaofitini ushukishwe cheo 

Wanaosema huwezi fika popote 


Waambie pole, pole pole 

Wanaotabiri, wanaokuwazia 

Watangoja sana 

Ninaye Yesu, nasonga mbele 

Nyuma sirudi tena 

Watangoja sana 


BweniEve Productions

Now Playing...