Ameshinda Yesu

By Boaz Danken

Lyrics

Kulikuwa na vita mbinguni 

Malaika wa Mungu 

Walipigana na yule joka 

Adui wa imani 


Wakamshinda kwa neno la ushuhuda 

Wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo 


Ameshinda Yesu kifo na kaburi 

Ameshinda Yesu mfalme wa amani 


Halleluya Halleluya 

Halleluya Halleluya 


Tumeingia kwenye agano 

Agano la milele 

Tumewekewa muhuri kwa damu 

Damu ya mwanakondoo 


Upande wetu sisi ni washindi 

Tumeshinda pamoja naye 

Kwa kumuamini Yesu kaingia moyoni 

Tutatawala pamoja naye 


Ameshinda Yesu kifo na kaburi 

Ameshinda Yesu mfalme wa amani 


Halleluya Halleluya 

Halleluya Halleluya 


Alizidi enzi mamlaka 

Kagongemelewa msalabani 

*Akaziuia mkoko alipokuwa Goligotha 

Adhabu Ya Mungu kwa wanadamu 

Ilikuwa begani mwake 

Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona 

Ushindi tunao 


Ameshinda Yesu kifo na kaburi 

Ameshinda Yesu mfalme wa amani 


Halleluya Halleluya 

Halleluya Halleluya 


Habari njema zienee 

Mataifa yasikie 

Mfalme wetu Yesu kristo 

Ameshinda kifo na kaburi 

Wivu wa Mungu umezidi 

Alikumbuka agano lake 

Uzao wa mwanamke 

Utakuponda kichwa wewe joka 

Yesu uzao wa mwanamke 

Amemponda kichwa joka shetani 

Tumeuona utukufu kama wa mwana pekee wa Mungu 

Yaliyonenwa na manabii torati na waamuzi 

Yametimia mikononi mwake 

Yesu mwana wa Mungu 


Ameshinda Yesu kifo na kaburi 

Ameshinda Yesu mfalme wa amani 

Boaz Danken- AMESHINDA YESU (official video)