Nisaidie Lyrics

By Fred Msungu

Lyrics

Mateso yakizidi hofu hutawala 

Hakuna tumaini lini yatakwisha 

Imani yatoweka hakuna tumaini 

Mungu wangu nisaidie 


Hakuna hata moja aniwazia mema 

Adui wamezidi rafiki wageuka 

Sioni hata moja wakunisaidia 

Baba wee Mungu wangu nisaidie 


Ninapoonewa ninapolemewa 

Giza likitanda nuru zikiisha 

Mungu wangu nisaidie 


Mungu nakungoja wewe 

Nipe nguvu mpya 

Nivuke kama tai 

Nitembee bila kuchoka 

Nipige mbio mbele bila kuzimia 

Mungu wangu nisaidie 


Nimeshajinyonyoa manyoya 

Nimeparua kwa mbali 

Nimepunguza uzito kwa bidii 

Niko tayari kuruka tena 

Maisha yangu ya pili nzuri 

Kulinganisha na yale ya kwanza 

Niko tayari ninazo nguvu kama tai 

Ujana wangu umerejea 

Maisha yangu yamerejea 

Sasa niko na nguvu 

Sioni wii tena haleluya 


Ninapoonewa ninapolemewa 

Giza likitanda nuru zikiisha 

Mungu wangu nisaidie 


Nisaidie nisaidie 

Nisaidie nisaidie 


Wale wangojao watapata nguvu mpya 

Watapaa juu kwa mbali kama tai 


Ninapoonewa ninapolemewa 

Giza likitanda nuru zikiisha 

Mungu wangu nisaidie 

Mungu wangu nisaidie 


Ninapoonewa ninapolemewa 

Giza likitanda nuru zikiisha 

Mungu wangu nisaidie 


Now Playing...