Msaada Wangu - Zaburi
Geraldine Oduor's 'Msaada Unatoka Kwa Mungu' is a Swahili Christian song that declares God as the source of help and protection. The lyrics echo Psalm 121, lifting eyes to the hills and affirming that help comes from the Lord. The song emphasizes God's faithfulness as a keeper who shields from harm day and night. It also celebrates the perfection of God's law and the sweetness of His judgments. The repeated refrain centers on trusting God alone for assistance, making it a worshipful declaration of dependence on God's care and guidance.
Msaada wangu watoka wapi
Msaada wangu kwako Bwana
Nakuinulia macho yangu
Wewe uketiye juu sana
Kama macho ya watumishi
Wa mkono wa Bwana zao
Nilitewe nuru yako
Kweli azidi kuniongoza
Zinifikishe kwenye mlima
Maskani yako takatifu
Bwana ndiye mlinzi wangu
Uvuli wa mkono wake
Jua halinipigi mchana
Wala mwezi usiku
Anilinda na mabaya
Atalinda nafsi yangu
Nitokapo na niingiapo
Tangu sasa na milele
Nitayainua macho yangu milimani
Msaada wangu watoka wapi?
Msaada wangu kwako Bwana
Sheria yako ni kamilifu
Huiburudisha nafsi yangu
Ushuhuda wako ni amini, hunitia hekima
Maagizo yako ni adili, hufurahisha nafsi yangu
Amri yako ni safi sana, huyatia macho huru
Kilicho chako ni kitakatifu, Kinadumu milele
Hukumu zako ni za kweli, zina haki kabisa
Kuliko wengi wa dhahabu, hukumu zako zatamanika
Kuliko sega za asali, hukumu zako tamu kweli
Nitayainua macho yangu milimani
Msaada wangu watoka wapi?
Msaada wangu kwako Bwana
Bass
Nitayainua macho yangu milimani
Wewe u msaada, wangu wa karibu