Nikumbushe Cover Lyrics

By Glory Shavu

Lyrics

Nirahisi kinywa kujawa na lawama tele

Pale mambo yanapoonekana hayaendi

ni ajabu sana namna moyo unahangaika

Ajabu sana moyo unavyoonyesha mashaka yakwamba

japokuwa Mungu anaishi ndani yangu kuna muda nahofu,

Japokuwa Mungu anaketi kati yetu kuna muda nahofu, ahh

nakumbuka wana wa Israel katika bahari yashamu

Japo walikatiza katikati ya bahari kwa ushindi,

Kwa nyimbo nyingi waliimba na kumsifu Bwanaa.

Lakini baada ya kuvuka na kuliona jagwa

yalibadilika mambo, manung'unikoo yalisimama

Na kusahau muujiza alotenda Bwana Mwanzo aah.

Eee MUNGU Nisaidie ee eeh


Nikumbushe wema wako nisije laumu

Nikumbushe ukuu wako wakati wa Magumu

Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu

Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,

Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Eeh ee MUNGU Nisaidie

Nisaidie kukumbuka baba yakwamba umenichora

Kiganjani mwako kati ya wengi walioko duniani eenh

na mimi umenionaa oooh ooo

Nikumbushe baba yakwamba ni wewe umeniponya nilipoumwa

Yakwamba ni wewe mlipaji wa ada yangu shuleni.

ouoh ooh Yakwamba kama ungeniacha hatua moja

nisingelifika nilipo ooh eee Babaa

umenikung'uta mavumbi, kung'uta

mavumbi mimi na kuniheshimisha.


Nikumbushe wema wako nisije laumu

Nikumbushe ukuu wako wakati wa Magumu

Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu

Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi

Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Nikumbushe wema wako nisije laumu

Nikumbushe ukuu wako wakati wa Magumu

Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu

Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi

Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Yesu nakutazama ninakuamini wewe

Fungua maisha yangu, nisaidie nisilalamike

Mbele zako, katika hali zote nijue upo

Umesema hutaniacha eeh Yahweh


Original Song: Nikumbushe Wema Wako by Angel B


Now Playing...