Namwandama Bwana - Amini Utii 17 Lyrics

By Magena Main Youth Choir

Lyrics

Namwandama Bwana kwa alilonena,

Njia yangu huning'azia;

Nikimridhisha atanidumisha

Taamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Giza sina kwangu wala hata wingu

Yeye mara huviondoa

Woga wasiwasi, sononeko basi.

Huamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Masumbuko yote, sikitiko lote;

Kwa mapenzi hunilipia,

Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki,

Taamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Mimi sitajua raha sawasawa

Ila yote yesu kumpa;

Napata fadhili na radhi kamili,

Taamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Nitamfurahisha na kumtumaini,

Majumbani na njia-njia;

Agizo natenda; nikitumwa hwenda,

Huamini nitii pia


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

Now Playing...