Nasubiri Bado Lyrics

By Peter Blessing

Lyrics

Kutwa nzima imepita nikiwa ata sina cha mfukoni 

Naumia hakika kwani ata marafiki nao siwaoni 

Kwenye wingu la giza sijapata ata faraja tumboni 

Koroboi ndo stima namweleza yule unayetoka moyoni 

Maisha haya kizunguzungu ni wapi tena sina pakutorokea 

Kwenye giza sioni nuru ni nini chanzo nabaki nikijiongelea 

Kama namwona mamangu uchochole ndio wimbo na ndo kikwazo 

Pekee yangu kwa hakika naangaziwa sana 

Machozi ndo yangu hata kunivika cha chini ndio langu pato 

Eeeh mola wangu eeeh eeh 


Mwenyezi mimi nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 

Nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 


Mbona mawazo yangu ndo hivo katu sichoki kufikiria 

Masikini moyo wangu 

Mzigo wangu ndo mzito sina ata wa kunisaidia 

Naja kwako mola wangu maumivu yangu yaokolee 

Toka zama sichoki kusota dili zangu zakutege 

Mara napata saa zingine nakosa nyumbani nategemewa 

Wamechoka wa kunikopesha wazidi niombea wasikate tamaa 

oooh ooh oooh 

Kama kufunga sio mwanzo ni mtindo mpaka nashindwa nini ndo chanzo 

Ndio maana nimeandika wimbo 

Matatizo yasiyokosa likizo kilio ndio yangu mtindo 

Ni maji yamefika kwa shingo aaih 

Kama namwona mamangu uchochole ndio wimbo na ndo kikwazo 

Pekee yangu kwa hakika naangaziwa sana 

Machozi ndo yangu hata kunivika cha chini ndio langu pato 

Eeeh mola wangu eeeh eeh 


Mwenyezi mimi nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 

Nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado (mwenyezi) 

Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 


Kupambana kidume sichoki 

Sala zangu nitume sichoki 

Siwasikizi wengine sichoki 

Ipo siku ntapata

Music Video

Now Playing...