46 Twae Wangu Uzima

By Sifa Music

Lyrics

Twae wangu uzima,

Sadaka ya daima;

Twae saa na siku,

Zikutukuze huku.


Twae mikono nayo

Ifanye upendavyo,

Twae yangu miguu

Kwa wongozi wako tu.


Twae sauti yangu,

Niimbe kwa Mungu tu;

Itwae na midomo,

Ijae neno lako.


Twae dhanabu pia,

Na yote ya dunia;

Twae yangu hekima,

Upendavyo tumia.


Nia itwae, Mungu,

Haitakuwa yangu;

Twae moyo; ni wako,

Uwe makazi yako.


Twae mapenzi yangu,

Sifa za moyo wangu;

Twae kabisa nafsi

Nniwe wako halisi.