Wimbo Ulio Bora Mlango 2 Song Of Songs

Wimbo Ulio Bora 2:1 SongOfSongs 2:1

Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni.

Wimbo Ulio Bora 2:2 SongOfSongs 2:2

Kama nyinyoro kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti.

Wimbo Ulio Bora 2:3 SongOfSongs 2:3

Kama mpera kati ya miti ya msituni, Kadhalika mpendwa wangu kati ya vijana. Naliketi kivulini mwake kwa furaha, Na matunda yake naliyaonja kuwa matamu.

Wimbo Ulio Bora 2:4 SongOfSongs 2:4

Akanileta mpaka nyumba ya karamu, Na bendera yake juu yangu ni mapenzi.

Wimbo Ulio Bora 2:5 SongOfSongs 2:5

Nishibisheni zabibu, niburudisheni kwa mapera, Kwa maana nimezimia kwa mapenzi.

Wimbo Ulio Bora 2:6 SongOfSongs 2:6

Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, Nao wa kuume unanikumbatia!

Wimbo Ulio Bora 2:7 SongOfSongs 2:7

Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.

Wimbo Ulio Bora 2:8 SongOfSongs 2:8

Sikiliza! Ni mpendwa wangu! Tazama, anakuja, Akiruka milimani, akichachawa vilimani.

Wimbo Ulio Bora 2:9 SongOfSongs 2:9

Mpendwa wangu ni kama paa, au ayala. Tazama, asimama nyuma ya ukuta wetu, Achungulia dirishani, atazama kimiani.

Wimbo Ulio Bora 2:10 SongOfSongs 2:10

Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,

Wimbo Ulio Bora 2:11 SongOfSongs 2:11

Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake;

Wimbo Ulio Bora 2:12 SongOfSongs 2:12

Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.

Wimbo Ulio Bora 2:13 SongOfSongs 2:13

Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.

Wimbo Ulio Bora 2:14 SongOfSongs 2:14

Hua wangu, mafichoni mwa jabali, Katika sitara za magenge, Nitazame uso wako, nisikie sauti yako, Maana sauti yako ni tamu na uso wako mzuri.

Wimbo Ulio Bora 2:15 SongOfSongs 2:15

Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.

Wimbo Ulio Bora 2:16 SongOfSongs 2:16

Mpendwa wangu ni wangu, na mimi ni wake; Hulisha kundi lake penye nyinyoro.

Wimbo Ulio Bora 2:17 SongOfSongs 2:17

Hata jua lipunge, na vivuli vikimbie, Unigeukie, mpendwa wangu, Nawe uwe kama paa, au ayala, Juu ya milima ya Betheri.