Wimbo Ulio Bora Mlango 6 Song Of Songs

Wimbo Ulio Bora 6:1 SongOfSongs 6:1

Mpendwa wako amekwenda wapi, Wewe uliye mzuri katika wanawake? Mpendwa wako amegeukia upande upi, Ili tumtafute pamoja nawe?

Wimbo Ulio Bora 6:2 SongOfSongs 6:2

Mpendwa wangu ameshukia bustani yake, Kwenye matuta ya rihani; Ili kulisha penye bustani, Ili kuchuma nyinyoro.

Wimbo Ulio Bora 6:3 SongOfSongs 6:3

Mimi ni wake mpendwa wangu, naye ni wangu, Hulisha kundi lake penye nyinyoro.

Wimbo Ulio Bora 6:4 SongOfSongs 6:4

Mpenzi wangu, u mzuri kama Tirza, Mwenye kupendeza kama Yerusalemu, Wa kutisha kama wenye bendera.

Wimbo Ulio Bora 6:5 SongOfSongs 6:5

Uyageuzie macho yako mbali nami, Kwa maana yamenitisha sana. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi, Wakijilaza mbavuni pa Gileadi.

Wimbo Ulio Bora 6:6 SongOfSongs 6:6

Meno yako kama kundi la kondoo, Wakipanda kutoka kuoshwa; Ambao kila mmoja amezaa mapacha, Wala hakuna aliyefiwa kati yao.

Wimbo Ulio Bora 6:7 SongOfSongs 6:7

Mashavu yako ni kama kipande cha komamanga, Nyuma ya barakoa yako.

Wimbo Ulio Bora 6:8 SongOfSongs 6:8

Wako malkia sitini, na masuria themanini, Na wanawali wasiohesabika;

Wimbo Ulio Bora 6:9 SongOfSongs 6:9

Hua wangu, mkamilifu wangu, ni mmoja tu, Mtoto wa pekee wa mamaye. Ndiye kipenzi chake aliyemzaa, Binti wakamwona wakamwita heri; Malkia na masuria nao wakamwona, Wakamsifu, wakisema,

Wimbo Ulio Bora 6:10 SongOfSongs 6:10

Ni nani huyu atazamaye kama alfajiri, Mzuri kama mwezi, safi kama jua, Wa kutisha kama wenye bendera?

Wimbo Ulio Bora 6:11 SongOfSongs 6:11

Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua.

Wimbo Ulio Bora 6:12 SongOfSongs 6:12

Kabla sijajua, roho yangu ilinileta Katikati ya magari ya wakuu wangu.

Wimbo Ulio Bora 6:13 SongOfSongs 6:13

Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame.