Chorus / Description :
Kaa nami ni usiku sana
Usiniache gizani Bwana
Msaada wako haukomi
Nili pekee yangu, kaa nami
Kaa nami ni usiku tena
Usiniache gizani Bwana
Msaada wako haukomi
Nili pekee yangu, kaa nami
Siku zetu hazikawii kwisha
Sioni la kunifurahisha
Hakuna ambacho hakikomi
Usiye na mwisho, kaa nami
Nina haja nawe kila saa
Sina mwingine wa kunifaa
Mimi nitaongozwa na nani
Ila wewe bwana, kaa nami
Sichi neno uwapo karibu
Nipatalo lote si taabu?
Kifo na kaburi haviumi
nitashinda kwako, kaa nami
Swahili HYMN for Abide with Me
Perfomed BY Angela Chibalonza
Nilalapo nikuone wewe (Hold Thou Thy cross before my closing eyes;)
Gizani mwote nimulikie (Shine through the gloom and point me to the skies.)
NUru za mbinguni hazikomi (Heaven?s morning breaks, and earth?s vain shadows flee;)
Siku zangu zote kaa nami (In life, in death, O Lord, abide with me.)