26 Yesu Unipendaye
Lyrics
Yesu unipendaye Kwako nakimbilia, Ni wewe utoshaye,
Mwovu akinijia; Yafiche ubavuni, Mwako maisha yangu;
Nifiikishe mbinguni Wokoe moyo wangu.
Ngome nyingine sina; Nategemea kwako.
Usinitupe Bwana, Nipe neema yako,
Ninakuamania Mwenye kuniwezesha;
Shari wanikingia, Vitani wanitosha.
Nakutaka Mpaji Vyote napata kwako;
Niwapo muhitaji, Utanijazi vyako;
Nao waangukao Wanyonge wape nguvu;
Poza wauguao, Uongoze vipofu.
Bwana umeniosha Moyo kwa damu yako;
Neema ya kutosha Yapatikana kwako;
Kwako Bwana naona Kisima cha uzima;
Mwangu moyoni Bwana, Bubujika daima.
Song Information
- Artist
- Angela Chibalonza
- Genre / Category
- praise
- Views
- 800