Nitakuwa Na Wewe Lyrics

By Beda Andrew

Lyrics

Kama ni kukupenda niko sawa 

Kuwa nawe niko sawa 

Niko tayari walimwengu wanitenge 

Kama kuwa nawe ni kushamba 

Kuishi nawe si kujanja 

Niko tayari walimwengu wanicheke 


Sababu ninaelewa nikiwa na wewe napata raha 

Ninaelewa kuishi na wewe ni furaha 

Ninelewa iyee ninaelewa oooh


Hata iweje wafanyeje wasemeje 

Mimi sitakuacha 

Hata iweje wafanyeje wasemeje mimi sitakuacha 

Nitakuwa na wewe (iyee) 

Nikae na wewe (iyee) 

Nitembee na wewe (milele) 

Mwokozi wangu 


Maneno neno ya wanadamu yanavunja moyo yanapotosha 

Dhumuni lake ni kunitenga mbali nawe 

Kwa damu uliyo mwaga msalabani ili mimi niwe wathamani 

Sio rahisi kwa mwanadamu kunitenga nawe  


Kwangu ninaelewa nikiwa na wewe napata raha 

Ninaelewa kuishi na wewe ni furaha 

Ninelewa iyee ninaelewa oooh 


Hata iweje wafanyeje wasemeje 

Mimi sitakuacha 

Hata iweje wafanyeje wasemeje mimi sitakuacha 

Nitakuwa na wewe (iyee) 

Nikae na wewe (iyee) 

Nitembee na wewe (milele) 

Mwokozi wangu 


Moyo wangu nimekukabidhi 

Na mwili wangu hekalu lako 

Wewe Bwana nimekubali ukae nami 

Nitakuwa nawe siku zote 

Milele na milele sitokuacha 

Nitakubali kuacha vyote nikufuate wewe 

Sababu ninaelewa, ninaelewa 

Ninaelewa 


Nitakuwa na wewe (iyee) 

Nikae na wewe (iyee) 

Nitembee na wewe (milele) 

Mwokozi wangu 

Beda Andrew - Nitakuwa Na Wewe (Official Music Video)

Now Playing...