Nimehesabu

By Christina Shusho

Lyrics

Nimehesabu na kuhesabu 

Nimehesabu na kuhesabu 

Nimeongeza na kutoa 

Nikazidisha na kugawanya 



Nimeona ni wewe 

Yesu ni wewe tu 

Hakuna mwingine 

Yesu ni wewe tu 


Pekee yako ni wewe 

Yesu ni wewe tu 

Hesabu zote nilizofanya 

Nimeona ni wewe tu 

Pekee yako ni wewe 

Ni wewe Yesu ni wewe tu 

Mwanzo mwisho ni wewe 

Ni wewe Yesu ni wewe tu 

Yesu ni wewe, ni wewe tu 


Nikukumbuka ulikonitoa 

Nikikumbuka ulionitendea 

Ninakumbuka magonjwa ulioniponya 

Ninakumbuka vita ulionipigania 

Ninakumbuka safari umenitembeza 

Ninakumbuka yale Mungu uliyotenda 


Ninasema ni wee, ninasema ni wewe tu 

Ni wewe, Yesu ni wewe, ni wewe tu 


Nani awezaye kutenda uliyotenda Bwana 

Nani angelipa garama ulionilipia 

Kumbe si wenye mbio washindao michezo 

Wala walio hodari washindao vitani 

Nimeona watumwa wakipanda farasi eh Bwana 

Wala si wenye hekima wapatao chakula 

Bwana nimejumulisha, nikatoa nikagawa 

Wewe sijaona mwingine eeh Bwana 


Wewe Bwana, ni wee, ni wewe tu 

Ni wewe, ni wewe tu


CHRISTINA SHUSHO - NIMEHESABU (OFFICIAL AUDIO)