Teta Nao Remix

By Christina Shusho

Lyrics

Eeeh Bwana utete nao wanao teta nami 

Upigane nao wanao pigana nami 

Eeeh Bwana utete nao wanao teta nami 

Upigane nao wanao pigana nami 

Ushike ngao na kinga usimame nami unisaidie 

Vuta we mkuki uwapige wanaonifuatia 

Uambie nafsi yangu mimi ni wokovu wako 

Wananiuliza mambo nisiyoyajua 


Eeh Bwana utete nao wanaoteta nami 

Pigana nao wanaopigana nami 

Eeh Bwana utete nao wanaoteta nami 

Pigana nao wanaopigana nami 


Wahaibishwe wafedheheshwe 

Warudishwe nyuma wanaotafuta nafsi yangu 

Wafadhaishwe wawe kama makapi 

Mbele yao pepo malaika wa Bwana waangushe chini 



Wananilipa mabaya badala ya mema 

Kutwa kucha waniwinda ili niteseke ee 

Niko ndani yako niweke eeh Mungu 

Ubavuni mwako nikumbatie Jehovah wangu 

Mkononi mwako niweke eeh Mungu 

Ubavuni mwako nikumbatie Jehovah wangu 


Eeh Bwana utete nao wanaoteta nami 

Upigane nao wanaopigana nami 

Eeh Bwana utete nao wanaoteta nami 

Upigane nao wanaopigana nami 


Njia yao iwe giza na utelezi 

Malaika wa Bwana akiwafuatia 

Uharibifu uwapate kwa ghafla  

Wa uharibifu aanguke ndani yake 

Mimi bure wasinisemange bure wasinibonge 

Na uovu wao aloficha umnase mwenyewe 

Bila sababu amenichimbia shimo nafsi yangu 

Mifupa yangu yote itasema 

"Bwana ni nani aliye kama wewe?" 

Na nafsi yangu itamfurahia Bwana 


Wapendeza Bwana wapendeza eeh Bwana wapendeza 

Katika hili najua utatenda 

Nitetee Bwana nitetee eeh Bwana nitetee 

Katika hili najua utatenda 

CHRISTINA SHUSHO Feat DREAMERS SINGERS - TETA NAO (Remix) SMS SKIZA 7635815 TO 811