Napenda Niwe Na Wewe Lyrics

By Emmanuel Mgogo

Lyrics

Mimi napenda niwe karibu nawewe 

Niwe na wewe 

Univute niwe karibu na wewe Bwana 

Mimi napendanga 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 

Niwe na wewe 

Univute niwe karibu na wewe Bwana 

Mimi napendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 

Kuwa karibu nawewe ninapendanga 

Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 

Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Nina haja nawewe Bwana 

Ninatamani ukae nami 

Sioni mwingine Bwana 

Sijapata mwingine ila niwewe 

wakunifaa mimi wakunitunza ila niwewe 

Tabibu wa karibu Bwana 

Usinipite pembeni Bwana 

Sina mwingine wa kunihurumia 

Pale ninapojongiwa na wanyan'ganyi 

Uwe karibu, Wewe ni msamaria mwema utanihudumia 

Utanifunga majeraha na kunifariji 

Unionyeshe pendo lako maana wanipenda 

Unionyeshe pendo lako maana wanipenda 

Sioni la kunifurahisha nikiwa mbali nawe Bwana 

Kama mtu naelewa udongoni nitasinya na kudhoofika 

Ninaomba univute niwe karibu nawe 

Kama mti uliopandwa kando kando ya maji 

Uzao matunda mazuri wala majani yake hayanyauki 

Kila nitendalo lifanikiwe Bwana naomba 


Wewe ni maji ya uzima 

Wewe ni maji yaliyo hai 

Kisima cha uzima na upendo 

Kama ayala wa porini ayatamanivyo maji 

Ndivyo nafsi yangu yakutamani wewe 

Fanya hima usichelewe 

Univute karibu nawe niwe nawewe 

Napendaaaa 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 

Niwe na wewe 

Univute niwe karibu na wewe Bwana 

Mimi napendanga 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 

Niwe na wewe 

Univute niwe karibu na wewe Bwana 

Mimi napendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 

Kuwa karibu nawewe ninapendanga 

Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 

Kuwa karibu nawewe ninapendanga 


Kukaa nawewe ni shauku pekee la moyo wangu Bwana 

Hapa nilipo sijaridhika natamani nipandishwe juu 

Univute karibu nawe 

Karibu zaidi ya jana 

Uwe nuru niangazie lengo lako kama maji 

Nizame kwenye kizima cha uwepo wako 

Nimesoma katika neno lako zaburi umesema 

Aketiye mahali pake pa siri pa aliye juu 

Atakaa katika uvuli wake mwenye enzi 

Ataokolewa na mitego ya adui 

Silaha zote na mishale haitofanikiwa 

Silaha zote na mishale haitofanikiwa 

Nichukue uniweke hapo Bwana 

Hili ni ombi la moyo wangu 

Niketishe kwenye uwepo wako 

Utuketishe kwenye uwepo wako 

Usiniache gizani Bwana 

pekee yangu siwezi 


Kaa nami karibu nami 

Ndani yangu nami ndani yako 

Univute karibu nawe 

mikononi mwako niwe salama 

Univute karibu nawe 

Niwe nawewe Bwana 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 

Niwe na wewe 

Univute niwe karibu na wewe Bwana 

Mimi napendanga 


Mimi napenda niwe karibu nawewe 

Niwe na wewe 

Univute niwe karibu na wewe Bwana 

Mimi napendanga 


Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 

Kuwa karibu nawewe ninapendanga 

Maana hapa nipo moyo nina kiu zaidi 

Kuwa karibu nawewe ninapendanga 

Emmanuel Mgogo - MIMI NAPENDA (Official Music Video)

Now Playing...