Yote Mema

By Joel Lwaga

Lyrics

Aaaaah Mema, aaah mema [x3]

Ni rahisi kukusifu 

Wakati wakati wa mazuri 

Ni rahisi kuku-shukuru 

Wakati yanapotokea mema 

Ila ni ngumu kuamini 

Kuwa hata na magumu nayo Mungu umeyaruhusu 

Kwa kuniwazia mema 


Umeruhusu mazuri nifurahi, tena nikushukuru 

Na mabaya ili niwe hodari, na kisha nikusifu 

Mbele umeniwekea fahari, haya ni ya muda tu 

Macho yangu yatazama mbali, uliko utukufu


Yote mema yote mema, Yote mema 

Hata magumu yana sababu,

Yote mema, Yote mema 

Sitalaumu sitakufuru 


Sasa nimejua kuwa, wewe uliyenipa samaki 

Ndiwe pia umetaka, wakati mwingine nipate nyoka 

Tena nimejua kuwa, wewe uliyenipa mkate 

Ndiwe pia umetaka, wakati mwingine nipate jiwe 


Umeruhusu mazuri nifurahi, tena nikushukuru 

Na mabaya ili niwe hodari, na kisha nikusifu 

Mbele umeniwekea fahari, haya ni ya muda tu 

Macho yangu yatazama mbali, uliko utukufu 


Yote mema yote mema, Yote mema 

Hata magumu yana sababu,

Yote mema, Yote mema 

Sitalaumu sitakufuru 


Nimejifunza kuwa na shibe tena 

Nimejifunza kuwa na njaa tena 

Kuwa nacho hata kuwa nacho 

Najua yote yanafanya kazi, ili kunipatia mema 

Yamefanyika kama kazi, ukamalifu wake


Yote mema yote mema, Yote mema 

Hata magumu yana sababu,

Yote mema, Yote mema 

Sitalaumu sitakufuru 


Yote mema yote mema, Yote mema 

Hata magumu yana sababu,

Yote mema, Yote mema 

Sitalaumu sitakufuru 

JOEL LWAGA - YOTE MEMA (Official Video)