Wageni

By Paul Clement

Lyrics

Katika maisha yangu nilipokea wageni,

Nikawakaribisha kwangu, wakafanya vitu vingi

Hawakuwa wa kudumu, walikuwa wapitaji

Ila moyo wa ukarimu, ukanisababishia machozi


Mgeni wa kwanza alikuwa ni uchungu, 

Akaniumiza, akanipa maumivu

Alipomaliza akaenda zake,


Mgeni wa pili alikuwa ni huzuni,

Huyu naye

Akanikosesha furaha,


Mgeni wa tatu alikuwa ni magonjwa,

Akanidhoofisha, akataka kuniua

Hakufanikiwa akaenda zake


Aliyefuata alininyima watoto

Jina lake tasa, naye alipita


Mgeni mmoja jina lake ni mauti

Akamchukua Ntimi, akaniachia jeraha


Mgeni mwingine jina lake hofu

Hakutaka nifanikiwe, akanipa fikra potofu


Nikajiona siwezi, tena nitafeli

Huyo naye alipita


Hawa ni wageni, tena wapitaji

Hawatadumu, watapita

Hawa ni wageni, tena wapitaji

Hawatadumu, watapita


Hakuna jambo lolote gumu

Litakalodumu kwenye maisha yako

Ila yote yatapita

Na yakishapita, 

Hayatarudi tena


Tough times never last,

But tough people do


Mapito siyo mambo magumu unayoyapitia kwenye maisha yako, 

Ila mapito ni mambo magumu yanayopita kwenye maisha yako, 

Ndiyo maana ninaita mapito, kwa kuwa yanapita tu, na yanapita kwenye maisha yako, 

Na yakishapita hayawezi kurudi tena, Hah


Magonjwa,

Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita

Uchungu, (Huzuni)

Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita

Mateso, (Changamoto)

Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita

(Hata dhiki)

Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita