Lyrics Page

Mfalme wa Amani

By Solomon Mukubwa

2,811 views Sep 5, 2026 updated Verified editorial review

Solomon Mukubwa opens "Mfalme Wa Amani" — King of Peace — by quoting David directly: "nilikuwa kijana sasa ni mzee," I was young and now I am old, and in all that time never seen the righteous forsaken. That's Psalm 37, almost word for word, used here as the evidence behind everything that follows. The song then turns pastoral, addressing someone crying specifically — usilie, don't weep — because the King of Peace has already heard it, already seen the difficulty, and can do what human help cannot. The recurring question, "ni uwezo gani unaompinga Yesu" — what power opposes Jesus — answers itself the way Paul does when he asks who can stand against those God is for. By the end the song widens outward, praying peace over homes, workplaces, and specifically Africa and America, turning a personal testimony about God's faithfulness into intercession for people the singer will never meet.

Lyrics Verified by Editorial Team
Daudi kasema, nilikuwa kijana sasa ni mzee
Daudi kasema, nilikuwa kijana sasa ni mzee
Sijawahi ona mwenye haki ameachwa mimi
Wala watoto wake kuombaomba mikate barabarani

Mungu ni mwaminifu, kwa ahadi zake wanadamu
Mungu ni mwaminifu, kwa ahadi zake si kama wanadamu
Akiongea Yesu ameongea,
Akikuahidia kitu, Baba ameahidi na ujasiri aah
Atatenda kwa wakati wake yoyoo
Ninamwita Bwana wa amani yeyeyee
Ninamwita mfalme wa amani bwaanaa
Ndio maana mimi ninaimba kwa sababu ya amani yake
Ni uwezo gani, uwezo gani unaompinga Yesu
Uwezo gani, uwezo gani, uwezo gani
Mfalme wa amani, mfalme wa amani uinuliwe
Wewe ni mwema, wewe ni mwema Bwana wangu

Usilie, usilie, usiliwe wewe
Usilie Bwana anakujua ndugu yangu
Amesikia kilio chako wewe mama
Unalia nini kwa wanadamu, mama yangu
Wanadamu hawatakusaidia na kitu
Wanadamu hawatakuwezesha kwa kitu chochote
Tunaye mmoja anayepanguza machozi ya watu wake
Ni yule mfalme wa amani
Ni yule aliyesema yote imekwisha
Mama unayoyapitia ni yeye anayeyaona
anajua shida yako mama yangu
Anajua magumu yako baba yangu
Ukiwa na shida usiende kwa waganga wa dunia
Ukiwa na magumu usiende kwa wafumu wa dunia

Muite mfalme wa amani, yeye anajibu maombi
Ni uwezo gani, uwezo gani unaompinga Baba
Uwezo gani, uwezo gani, uwezo gani

Mfalme wa amani, uinuliwe Bwana wangu
Yale unayotenda inashangaza dunia nzima
Wanaokosa amani ndani ya nyumba zao wape amani
Wanaokosa amani ndani ya kazi zao wape amani
Ni wewe Bwana wa amani ya kudumu
Ni wewe Bwana wa amani ya Afrika
Amerika wanalia amani
Tunawe Bwana mfalme wa amani
Hakuna kitu kile kinachokushinda Bwana

Yeye Mfalme wa Amani uinuliwe
Wewe ni mwema, wewe ni mwema Bwana wangu

Music Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.