Lyrics Page

Usifurahi Juu Yangu eeh Adui

By Upendo Nkone

2,864 views Jun 6, 2026 updated
Usifurahi juu yangu eeeh adui yangu,
niangukapo mimi nitasimama tena.
Kumbuka niwapo gizani bwana nuru yangu,
hawezi kuniacha bwana mimi niangamie.

Si vyema kunisema vibaya nipatapo tatizo,
shetani wampa nafasi ndani ya moyo wako
Kumbuka kwa maombi yako nitasimama tena,
na utapata baraka kutoka kwake Mungu

Maana heri mtu yule ambaye kinywa chake,
huwabariki wenzake na kuwaombea.
Maana maneno mabaya huuchafua moyo.
kukuweka mbali na Mungu ni vema uwe safi.

Ukiona nipo kwenye shida (niombee),
Ndoa yangu imevunjika wewe niombee,
Nikifukuzwa kazini ndugu niombee,
Magonjwa yananiandama niombee,
Biashara haina faida niombee,
Nikikawia kupata mtoto nimbee,
Nimekuwa mtoto yatima niombee,
Hata nijapokuwa mjane niombee,

Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena,
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa,
Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena,
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa,

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.