2 Mambo ya Nyakati Mlango 17 2nd Chronicles
2 Mambo ya Nyakati 17:1 2ndChronicles 17:1
Na Yehoshafati mwanawe akatawala mahali pake, akajitia nguvu juu ya Israeli.
2 Mambo ya Nyakati 17:2 2ndChronicles 17:2
Akaweka jeshi katika miji yote yenye maboma ya Yuda, akatia na askari walinzi katika nchi ya Yuda, na katika miji ya Efraimu, aliyoitwaa Asa babaye.
2 Mambo ya Nyakati 17:3 2ndChronicles 17:3
Naye Bwana alikuwa pamoja na Yehoshafati, kwa kuwa alikwenda katika njia za kwanza za Daudi babaye, asiyatafute mabaali;
2 Mambo ya Nyakati 17:4 2ndChronicles 17:4
lakini alimtafuta Mungu wa baba yake, akaenda katika amri zake, wala si katika matendo ya Israeli.
2 Mambo ya Nyakati 17:5 2ndChronicles 17:5
Kwa hiyo Bwana akauthibitisha ufalme mkononi mwake; Yehoshafati akaletewa zawadi na Yuda wote; basi akawa na mali na heshima tele.
2 Mambo ya Nyakati 17:6 2ndChronicles 17:6
Ukainuliwa moyo wake katika njia za Bwana; na zaidi ya hayo akapaondoa mahali pa juu, na maashera, katika Yuda.
2 Mambo ya Nyakati 17:7 2ndChronicles 17:7
Tena, katika mwaka wa tatu wa kutawala kwake, akawatuma wakuu wake, yaani, Ben-haili, na Obadia, na Zekaria, na Nethaneli, na Mikaya, ili kufundisha mijini mwa Yuda;
2 Mambo ya Nyakati 17:8 2ndChronicles 17:8
na pamoja nao Walawi, yaani, Shemaya, na Nethania, na Zebadia, na Asaheli, na Shemiramothi, na Yehonathani, na Adonia, na Tobia, na Tob-adonia, Walawi; na pamoja nao Elishama na Yehoramu, makuhani.
2 Mambo ya Nyakati 17:9 2ndChronicles 17:9
Wakafundisha katika Yuda, wenye kitabu cha torati ya Bwana; wakazunguka katika miji yote ya Yuda, wakafundisha kati ya watu.
2 Mambo ya Nyakati 17:10 2ndChronicles 17:10
Hofu ya Bwana ikaziangukia falme za nchi zote zilizozunguka Yuda, wasipigane vita na Yehoshafati.
2 Mambo ya Nyakati 17:11 2ndChronicles 17:11
Na baadhi ya Wafilisti walimletea Yehoshafati zawadi, na fedha ya kodi; Waarabu nao wakamletea makundi, kondoo waume saba elfu na mia saba, na mabeberu saba elfu na mia saba.
2 Mambo ya Nyakati 17:12 2ndChronicles 17:12
Ukuu wake Yehoshafati ukazidi sana; akajenga katika Yuda ngome na miji ya hazina.
2 Mambo ya Nyakati 17:13 2ndChronicles 17:13
Naye alikuwa na kazi nyingi katika miji ya Yuda; na watu wa vita, watu mashujaa humo Yerusalemu.
2 Mambo ya Nyakati 17:14 2ndChronicles 17:14
Na hivi ndivyo walivyohesabiwa kwa mbari za baba zao; wa Yuda, maakida wa maelfu; Adna jemadari, na pamoja naye watu mashujaa mia tatu elfu;
2 Mambo ya Nyakati 17:15 2ndChronicles 17:15
na wa pili wake Yehohanani akida, na pamoja naye mia mbili na themanini elfu;
2 Mambo ya Nyakati 17:16 2ndChronicles 17:16
na baada yake Amasia mwana wa Zikri, aliyejitoa kwa Bwana kwa moyo, na pamoja naye mia mbili elfu, watu mashujaa;
2 Mambo ya Nyakati 17:17 2ndChronicles 17:17
na wa Benyamini; Eliada mtu shujaa, na pamoja naye mia mbili elfu wenye nyuta na ngao;
2 Mambo ya Nyakati 17:18 2ndChronicles 17:18
na wa pili wake Yehozabadi, na pamoja naye mia na themanini elfu waliojiweka tayari kwa vita.
2 Mambo ya Nyakati 17:19 2ndChronicles 17:19
Hao ndio waliomngojea mfalme, zaidi ya hao mfalme aliowaweka katika miji yenye maboma katika Yuda yote.