2 Mambo ya Nyakati Mlango 12 2nd Chronicles

2 Mambo ya Nyakati 12:1 2ndChronicles 12:1

Ikawa ulipothibitika ufalme wa Rehoboamu, naye amepata nguvu, aliiacha torati ya Bwana, na Israeli wote pamoja naye.

2 Mambo ya Nyakati 12:2 2ndChronicles 12:2

Ikawa katika mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu, akapanda Shishaki, mfalme wa Misri, juu ya Yerusalemu; kwa kuwa walikuwa wamemwasi Bwana;

2 Mambo ya Nyakati 12:3 2ndChronicles 12:3

mwenye magari elfu moja na mia mbili, na wapanda farasi sitini elfu; na watu wasiohesabika, waliotoka Misri pamoja naye; Walubi, na Wasukii, na Wakushi.

2 Mambo ya Nyakati 12:4 2ndChronicles 12:4

Akaitwaa miji yenye maboma iliyokuwa ya Yuda, akaja Yerusalemu.

2 Mambo ya Nyakati 12:5 2ndChronicles 12:5

Ndipo akaja Shemaya nabii kwa Rehoboamu, na kwa wakuu wa Yuda, waliokusanyika Yerusalemu kwa sababu ya Shishaki, akawaambia, Bwana asema hivi, Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo nami nimewaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.

2 Mambo ya Nyakati 12:6 2ndChronicles 12:6

Ndipo wakajinyenyekeza wakuu wa Israeli na mfalme; wakasema, Bwana ndiye mwenye haki.

2 Mambo ya Nyakati 12:7 2ndChronicles 12:7

Naye Bwana alipoona ya kwamba wamejinyenyekeza, neno la Bwana likamjia Shemaya, kusema, Wamejinyenyekeza; sitawaharibu; lakini nitawapa wokovu punde, wala ghadhabu yangu haitamwagika juu ya Yerusalemu kwa mkono wa Shishaki.

2 Mambo ya Nyakati 12:8 2ndChronicles 12:8

Walakini watamtumikia; ili wapate kujua utumwa wangu, na huo utumwa wa falme za nchi.

2 Mambo ya Nyakati 12:9 2ndChronicles 12:9

Basi Shishaki, mfalme wa Misri, akapanda juu ya Yerusalemu, akazichukua hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za nyumba ya mfalme; akazichukua zote. Akazichukua pia ngao za dhahabu alizozifanya Sulemani.

2 Mambo ya Nyakati 12:10 2ndChronicles 12:10

Mfalme Rehoboamu akafanya ngao za shaba mahali pake, akawakabidhi wakuu wa walinzi, waliongoja mlangoni pa nyumba ya mfalme.

2 Mambo ya Nyakati 12:11 2ndChronicles 12:11

Ikawa kila wakati mfalme alipoingia nyumbani mwa Bwana, wakaja walinzi wakazichukua, wakazirudisha tena chumbani mwa walinzi.

2 Mambo ya Nyakati 12:12 2ndChronicles 12:12

Naye alipojinyenyekeza, ghadhabu ya Bwana ikamgeukia mbali, asimharibu kabisa; tena yalionekana katika Yuda mambo mema.

2 Mambo ya Nyakati 12:13 2ndChronicles 12:13

Basi mfalme Rehoboamu akajitia nguvu katika Yerusalemu, akatawala; maana Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke huko jina lake. Na jina la mamaye aliitwa Naama Mwamoni.

2 Mambo ya Nyakati 12:14 2ndChronicles 12:14

Naye akatenda yaliyo maovu, kwa kuwa hakuukaza moyo wake amtafute Bwana.

2 Mambo ya Nyakati 12:15 2ndChronicles 12:15

Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.

2 Mambo ya Nyakati 12:16 2ndChronicles 12:16

Rehoboamu akalala na babaze, akazikwa katika mji wa Daudi. Na Abiya mwanawe alitawala mahali pake.