2 Mambo ya Nyakati Mlango 4 2nd Chronicles
2 Mambo ya Nyakati 4:1 2ndChronicles 4:1
Tena akafanya madhabahu ya shaba, mikono ishirini urefu wake, na mikono ishirini upana wake, na mikono kumi kwenda juu kwake.
2 Mambo ya Nyakati 4:2 2ndChronicles 4:2
Tena akaifanya bahari ya kusubu, mikono kumi toka ukingo hata ukingo, ya mviringo, na kwenda juu kwake ilikuwa mikono mitano; na uzi wa mikono thelathini kuizunguka kabisa.
2 Mambo ya Nyakati 4:3 2ndChronicles 4:3
Na chini yake palikuwa na mifano ya ng'ombe, walioizunguka pande zote ,kwa mikono kumi,wakiizunguka pande zote ile bahari. Ng`ombe walikuwa safu mbili ,wakayeyushwa hapo ilipoyeyushwa hiyo bahari.
2 Mambo ya Nyakati 4:4 2ndChronicles 4:4
Ikakaa juu ya ng'ombe kumi na wawili, watatu wakitazama kaskazini, na watatu wakitazama magharibi, na watatu wakitazama kusini, na watatu wakitazama mashariki; na bahari iliwekwa juu yao, na pande zao za nyuma zote zilikuwa ndani.
2 Mambo ya Nyakati 4:5 2ndChronicles 4:5
Na unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ukafanywa kama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi; huingia bathi elfu tatu, kukaa ndani yake.
2 Mambo ya Nyakati 4:6 2ndChronicles 4:6
Akafanya na birika kumi, akaziweka tano upande wa kuume, na tano upande wa kushoto, za kuoshea; ndizo walizooshea mambo ya kafara; lakini hiyo bahari ilikuwa ya makuhani ya kuogea.
2 Mambo ya Nyakati 4:7 2ndChronicles 4:7
Akavifanya vinara vya taa kumi vya dhahabu, kadiri ya vilivyoagiziwa; akavitia hekaluni, vitano upande wa kuume, na vitano upande wa kushoto.
2 Mambo ya Nyakati 4:8 2ndChronicles 4:8
Akafanya na meza kumi, akazitia hekaluni, tano upande wa kuume, na tano upande wa kushoto. Kisha akafanya mabakuli mia ya dhahabu.
2 Mambo ya Nyakati 4:9 2ndChronicles 4:9
Tena akaufanya ua wa makuhani, na ua mkubwa, nayo milango yake, akaifunikiza kwa shaba milango yake.
2 Mambo ya Nyakati 4:10 2ndChronicles 4:10
Nayo bahari akaiweka upande wa kuume kwa mashariki, kuelekea kusini.
2 Mambo ya Nyakati 4:11 2ndChronicles 4:11
Na Huramu akayafanya masufuria, na majembe, na mabakuli. Basi Huramu akamaliza kufanya hiyo kazi, aliyomfanyia mfalme Sulemani ya nyumba ya Mungu;
2 Mambo ya Nyakati 4:12 2ndChronicles 4:12
zile nguzo mbili, na vimbe, na taji mbili zilizokuwa juu ya nguzo; nazo nyavu mbili za kuzifunika vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo;
2 Mambo ya Nyakati 4:13 2ndChronicles 4:13
na makomamanga mia nne ya nyavu mbili; safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, kuzifunika vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo.
2 Mambo ya Nyakati 4:14 2ndChronicles 4:14
Akayafanya na matako, na mabirika akafanya juu ya matako;
2 Mambo ya Nyakati 4:15 2ndChronicles 4:15
bahari moja, na ng'ombe kumi na wawili chini yake.
2 Mambo ya Nyakati 4:16 2ndChronicles 4:16
Masufuria pia, na majembe, na nyuma, na vyombo vyake vyote, Huramu akamfanyia mfalme Sulemani kwa nyumba ya BWANA ,vya shaba iliyokatuka.
2 Mambo ya Nyakati 4:17 2ndChronicles 4:17
Katika uwanda wa Yordani ndipo mfalme alipovisubu, katika udongo mzito kati ya Sukothi na Sereda.
2 Mambo ya Nyakati 4:18 2ndChronicles 4:18
Ndivyo alivyovifanya Sulemani vyombo hivyo vyote, vingi sana; kwa kuwa uzani wa shaba ulikuwa hautafutikani.
2 Mambo ya Nyakati 4:19 2ndChronicles 4:19
Basi Sulemani akavifanya vyombo vyote vilivyokuwamo nyumbani mwa Mungu, madhabahu ya dhahabu pia, nazo meza, ambazo juu yake iliwekwa mikate ya wonyesho;
2 Mambo ya Nyakati 4:20 2ndChronicles 4:20
na vinara na taa zake, ziwake kama ilivyoagizwa mbele ya chumba cha ndani, vya dhahabu iliyosafika;
2 Mambo ya Nyakati 4:21 2ndChronicles 4:21
na maua, na taa, na makoleo, ya dhahabu, ndiyo dhahabu bora;
2 Mambo ya Nyakati 4:22 2ndChronicles 4:22
na mikasi, na mabakuli, na miiko, na vyetezo, vya dhahabu iliyosafika; na kwa habari za mahali pa kuingia nyumbani, milango yake ya ndani ya patakatifu pa patakatifu, na milango ya nyumba, yaani ya hekalu, ilikuwa ya dhahabu.