2 Mambo ya Nyakati Mlango 3 2nd Chronicles

2 Mambo ya Nyakati 3:1 2ndChronicles 3:1

Ndipo Sulemani akaanza kuijenga nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, juu ya mlima Moria, pale Bwana alipomtokea Daudi babaye alipotengeza mahali pale alipoagiza Daudi, katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.

2 Mambo ya Nyakati 3:2 2ndChronicles 3:2

Akaanza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa kutawala kwake.

2 Mambo ya Nyakati 3:3 2ndChronicles 3:3

Basi hii ndiyo misingi ya majengo ya nyumba ya Mungu aliyoiweka Sulemani. Urefu wake kwa mikono ya cheo cha kwanza ulikuwa mikono sitini, na upana wake mikono ishirini.

2 Mambo ya Nyakati 3:4 2ndChronicles 3:4

Na ukumbi uliokuwa mbele yake, urefu wake kadiri ya upana wa nyumba ulikuwa mikono ishirini, na kwenda juu kwake mia na ishirini; akaufunikiza ndani kwa dhahabu safi.

2 Mambo ya Nyakati 3:5 2ndChronicles 3:5

Nayo nyumba kubwa akaifunika miti ya miberoshi, aliyoifunikiza kwa dhahabu safi, akaifanyizia mitende na minyororo.

2 Mambo ya Nyakati 3:6 2ndChronicles 3:6

Akaipamba nyumba kwa vito iwe na uzuri; nayo dhahabu ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.

2 Mambo ya Nyakati 3:7 2ndChronicles 3:7

Tena, akaifunikiza kwa dhahabu nyumba, na boriti, na vizingiti, na kuta zake, na milango yake; akachora makerubi kutani.

2 Mambo ya Nyakati 3:8 2ndChronicles 3:8

Akaifanya nyumba ya patakatifu pa patakatifu; urefu wake kadiri ya upana wa nyumba, ulikuwa mikono ishirini, na upana wake mikono ishirini; akaifunikiza kwa dhahabu safi, ya talanta mia sita.

2 Mambo ya Nyakati 3:9 2ndChronicles 3:9

Na uzani wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Akazifunikiza orofa zake za juu kwa dhahabu.

2 Mambo ya Nyakati 3:10 2ndChronicles 3:10

Na ndani ya nyumba ya patakatifu pa patakatifu akafanyiza makerubi mawili ya kuchonga; wakayafunikiza kwa dhahabu.

2 Mambo ya Nyakati 3:11 2ndChronicles 3:11

Na mabawa ya makerubi hayo urefu wake ulikuwa mikono ishirini; bawa moja mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la pili.

2 Mambo ya Nyakati 3:12 2ndChronicles 3:12

Na bawa la kerubi la pili lilikuwa mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la kwanza.

2 Mambo ya Nyakati 3:13 2ndChronicles 3:13

Yakaenea mabawa ya makerubi hayo mikono ishirini; yakasimama juu ya miguu yao, na nyuso zao ziliielekea nyumba.

2 Mambo ya Nyakati 3:14 2ndChronicles 3:14

Akalifanya pazia la samawi na urujuani na nyekundu, na kitani safi, akaifanyizia makerubi.

2 Mambo ya Nyakati 3:15 2ndChronicles 3:15

Tena akafanya mbele ya nyumba nguzo mbili za mikono thelathini na tano kwenda juu kwake, na taji iliyokuwa juu yake moja moja ilikuwa mikono mitano.

2 Mambo ya Nyakati 3:16 2ndChronicles 3:16

Akafanya minyororo ndani ya chumba cha ndani, akaiweka juu ya vichwa vya nguzo; akafanya makomamanga mia, akayaweka juu ya hiyo minyororo.

2 Mambo ya Nyakati 3:17 2ndChronicles 3:17

Akazisimamisha nguzo hizo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume, na ya pili upande wa kushoto; akaliita jina la ile ya kuume Yakini, na jina la ile ya kushoto Boazi.