2 Mambo ya Nyakati Mlango 13 2nd Chronicles
2 Mambo ya Nyakati 13:1 2ndChronicles 13:1
Katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu, akaanza Abiya kutawala juu ya Yuda.
2 Mambo ya Nyakati 13:2 2ndChronicles 13:2
Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka binti Urieli wa Gibea. Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
2 Mambo ya Nyakati 13:3 2ndChronicles 13:3
Abiya akapanga vita mwenye jeshi la watu hodari wa vita, watu wateule mia nne elfu; naye Yeroboamu akapanga vita juu yake mwenye watu wateule mia nane elfu, waliokuwa waume mashujaa.
2 Mambo ya Nyakati 13:4 2ndChronicles 13:4
Basi Abiya akasimama juu ya kilima cha Semaraimu, kilichoko milimani mwa Efraimu, akasema, Nisikieni, enyi Yeroboamu na Israeli wote;
2 Mambo ya Nyakati 13:5 2ndChronicles 13:5
je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?
2 Mambo ya Nyakati 13:6 2ndChronicles 13:6
Lakini Yeroboamu mwana wa Nebati, mtumwa wa Sulemani mwana wa Daudi, akainuka, akamfanyia fitina bwana wake.
2 Mambo ya Nyakati 13:7 2ndChronicles 13:7
Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, wasiofaa kitu, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia.
2 Mambo ya Nyakati 13:8 2ndChronicles 13:8
Hata sasa mwajidhania kuwa mtauzuia ufalme wa Bwana mikononi mwa wana wa Daudi; nanyi mmekuwa jamii kubwa, na kwenu mna ndama za dhahabu alizowafanyia Yeroboamu kuwa miungu.
2 Mambo ya Nyakati 13:9 2ndChronicles 13:9
Je! Hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Haruni, na Walawi; mkajifanyia makuhani kama wafanyavyo watu wa nchi nyingine? Hata ye yote ajaye kujifanya wakfu na ndama, na kondoo waume saba, aweza kuwa kuhani wa hiyo isiyo miungu.
2 Mambo ya Nyakati 13:10 2ndChronicles 13:10
Lakini sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala sisi hatukumwacha; tena tunao makuhani wanaomtumikia Bwana, wana wa Haruni, na Walawi, kwa kazi yao;
2 Mambo ya Nyakati 13:11 2ndChronicles 13:11
nao humtolea Bwana kila asubuhi, na kila jioni, sadaka za kuteketezwa na fukizo la manukato; mikate ya wonyesho pia huiweka kwa taratibu yake juu ya meza takatifu, na kinara cha dhahabu chenye taa zake, kuwaka kila jioni; kwa maana sisi twayalinda malinzi ya Bwana, Mungu wetu; bali ninyi mmemwacha.
2 Mambo ya Nyakati 13:12 2ndChronicles 13:12
Na tazama, Mungu yu pamoja nasi atutangulie, na makuhani wake wenye mapanda, ili wapige sauti ya kugutusha juu yenu. Enyi wana wa Israeli, msipigane na Bwana, Mungu wa baba zenu; kwani hamtafanikiwa.
2 Mambo ya Nyakati 13:13 2ndChronicles 13:13
Lakini Yeroboamu aliwazungushia waviziao kwa nyuma; basi wao wakawa mbele ya Yuda, na wale waviziao nyuma yao.
2 Mambo ya Nyakati 13:14 2ndChronicles 13:14
Na Yuda walipotazama nyuma, angalia, vita vikawa mbele na nyuma; wakamlilia Bwana, na makuhani wakapiga mapanda.
2 Mambo ya Nyakati 13:15 2ndChronicles 13:15
Ndipo wakapiga kelele watu wa Yuda; ikawa, watu na Yuda walipopiga kelele, Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda.
2 Mambo ya Nyakati 13:16 2ndChronicles 13:16
Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao.
2 Mambo ya Nyakati 13:17 2ndChronicles 13:17
Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule.
2 Mambo ya Nyakati 13:18 2ndChronicles 13:18
Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Mambo ya Nyakati 13:19 2ndChronicles 13:19
Abiya akamfuata Yeroboamu, akamnyang'anya miji, Betheli na miji yake, na Yeshana na miji yake, na Efroni na miji yake.
2 Mambo ya Nyakati 13:20 2ndChronicles 13:20
Wala Yeroboamu hakupata nguvu tena siku za Abiya; kisha Bwana akampiga, akafa.
2 Mambo ya Nyakati 13:21 2ndChronicles 13:21
Ila Abiya akapata nguvu, akaoa wake kumi na wanne, akazaa wana ishirini na wawili, na binti kumi na sita.
2 Mambo ya Nyakati 13:22 2ndChronicles 13:22
Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.