2 Mambo ya Nyakati Mlango 8 2nd Chronicles

2 Mambo ya Nyakati 8:1 2ndChronicles 8:1

Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani aliijenga nyumba ya Bwana, na nyumba yake mwenyewe;

2 Mambo ya Nyakati 8:2 2ndChronicles 8:2

ndipo Sulemani akaijenga miji ile Hiramu aliyompa Sulemani, akawakalisha humo wana wa Israeli.

2 Mambo ya Nyakati 8:3 2ndChronicles 8:3

Naye Sulemani akaenda Hamath-zoba, akaushinda.

2 Mambo ya Nyakati 8:4 2ndChronicles 8:4

Akaujenga Tadmori wa nyikani, na miji yote ya hazina, aliyoijenga katika Hamathi.

2 Mambo ya Nyakati 8:5 2ndChronicles 8:5

Tena akaujenga Beth-horoni wa juu, na Beth-horoni wa chini, miji yenye boma, yenye kuta, na malango, na makomeo;

2 Mambo ya Nyakati 8:6 2ndChronicles 8:6

na Baalathi, na miji yote ya hazina Sulemani aliyokuwa nayo, na miji yote ya magari yake, na miji ya wapanda farasi wake, na ya anasa yote aliyopenda Sulemani kujenga humo Yerusalemu, na katika Lebanoni, na katika nchi yote ya mamlaka yake.

2 Mambo ya Nyakati 8:7 2ndChronicles 8:7

Basi kwa habari ya watu wote waliosalia wa Wahiti, na wa Waamori, na wa Waperizi, na wa Wahivi, na wa Wayebusi, wasiokuwa wa Israeli;

2 Mambo ya Nyakati 8:8 2ndChronicles 8:8

wa watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuwakomesha, katika hao Sulemani akawatumikisha shokoa hata leo.

2 Mambo ya Nyakati 8:9 2ndChronicles 8:9

Wala katika wana wa Israeli Sulemani hakuwafanya watumwa kazini mwake; lakini hao walikuwa watu wa vita, na wakuu wa majemadari wake, na maakida wa magari yake na wa wapanda farasi wake.

2 Mambo ya Nyakati 8:10 2ndChronicles 8:10

Na hao walikuwa maakida wakuu wa Sulemani, watu mia mbili na hamsini, waliotawala juu ya watu.

2 Mambo ya Nyakati 8:11 2ndChronicles 8:11

Sulemani akamleta binti Farao kutoka mji wa Daudi mpaka nyumba aliyomjengea; kwa kuwa alisema, Mke wangu hatakaa nyumbani mwa Daudi mfalme wa Israeli, kwa kuwa ni patakatifu, mahali palipofika sanduku la Bwana.

2 Mambo ya Nyakati 8:12 2ndChronicles 8:12

Ndipo Sulemani akamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, aliyoijenga mbele ya ukumbi,

2 Mambo ya Nyakati 8:13 2ndChronicles 8:13

kadiri ilivyohitajiwa huduma ya kila siku, akitoa sawasawa na amri ya Musa, siku za sabato, na za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoamriwa, mara tatu kila mwaka, yaani, sikukuu ya mikate isiyochachwa, na sikukuu ya majuma, na sikukuu ya vibanda.

2 Mambo ya Nyakati 8:14 2ndChronicles 8:14

Akaziamuru, sawasawa na agizo la Daudi babaye, zamu za makuhani za kutumika, nao Walawi kwa kadiri ya malinzi yao, ili kusifu, na kuhudumu mbele ya makuhani, kama ilivyohitajiwa kila siku; tena mabawabu kwa zamu zao za kila mlango; maana ndivyo alivyoamuru Daudi mtu wa Mungu.

2 Mambo ya Nyakati 8:15 2ndChronicles 8:15

Wala hawakuyaacha maagizo ya mfalme aliyowaamuru makuhani na Walawi kwa neno lo lote, wala kwa habari ya hazina.

2 Mambo ya Nyakati 8:16 2ndChronicles 8:16

Basi ikatengenezwa kazi yote ya Sulemani hata siku ya kutiwa msingi wa nyumba ya Bwana, na hata ilipokwisha. Hivyo ikamalizika nyumba ya Bwana.

2 Mambo ya Nyakati 8:17 2ndChronicles 8:17

Ndipo Sulemani akaenda Esion-geberi, na Elothi, pwani ya nchi ya Edomu.

2 Mambo ya Nyakati 8:18 2ndChronicles 8:18

Naye Hiramu akamletea merikebu kwa mikono ya watumishi wake, na watumishi waliokuwa wana-maji; nao wakafika Ofiri pamoja na watumishi wa Sulemani, wakachukua kutoka huko talanta mia nne na hamsini za dhahabu, wakamletea mfalme Sulemani.