2 Wakorintho Mlango 13 2nd Corinthians
2 Wakorintho 13:1 2ndCorinthians 13:1
Hii ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.
2 Wakorintho 13:2 2ndCorinthians 13:2
Nimetangulia kuwaambia; na, kama vile nilipokuwapo mara ya pili, vivyo hivyo sasa nisipokuwapo, nawaambia wazi wao waliotenda dhambi tangu hapo, na wengine wote, ya kwamba, nikija, sitahurumia;
2 Wakorintho 13:3 2ndCorinthians 13:3
kwa kuwa mnatafuta dalili ya Kristo, asemaye ndani yangu, ambaye si dhaifu kwenu, bali ana uweza ndani yenu.
2 Wakorintho 13:4 2ndCorinthians 13:4
Maana, alisulibiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Maana sisi nasi tu dhaifu katika yeye; lakini tutaishi pamoja naye kwa uweza wa Mungu ulio kwenu.
2 Wakorintho 13:5 2ndCorinthians 13:5
Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.
2 Wakorintho 13:6 2ndCorinthians 13:6
Lakini natumaini kama mtajua ya kuwa sisi hatukukataliwa.
2 Wakorintho 13:7 2ndCorinthians 13:7
Nasi twamwomba Mungu, msifanye lo lote lililo baya; si kwamba sisi tuonekane tumekubaliwa, lakini ninyi mfanye lile lililo jema, tujapokuwa sisi tu kama waliokataliwa.
2 Wakorintho 13:8 2ndCorinthians 13:8
Maana hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli.
2 Wakorintho 13:9 2ndCorinthians 13:9
Maana twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa hodari. Tena twaomba hili nalo, kutimilika kwenu.
2 Wakorintho 13:10 2ndCorinthians 13:10
Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo, ili, nikiwapo, nisiutumie ukali kwa kadiri ya uwezo ule niliopewa na Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa.
2 Wakorintho 13:11 2ndCorinthians 13:11
Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
2 Wakorintho 13:12 2ndCorinthians 13:12
Salimianeni kwa busu takatifu.
2 Wakorintho 13:13 2ndCorinthians 13:13
Watakatifu wote wawasalimu.
2 Wakorintho 13:14 2ndCorinthians 13:14
Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.