2 Wakorintho Mlango 11 2nd Corinthians
2 Wakorintho 11:1 2ndCorinthians 11:1
Laiti mngechukuliana nami katika upumbavu wangu kidogo! Naam, mchukuliane nami.
2 Wakorintho 11:2 2ndCorinthians 11:2
Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.
2 Wakorintho 11:3 2ndCorinthians 11:3
Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.
2 Wakorintho 11:4 2ndCorinthians 11:4
Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!
2 Wakorintho 11:5 2ndCorinthians 11:5
Maana nadhani ya kuwa mimi sikupungukiwa na kitu walicho nacho mitume walio wakuu.
2 Wakorintho 11:6 2ndCorinthians 11:6
Lakini nijapokuwa mimi ni mtu asiyejua kunena, hii si hali yangu katika elimu; ila katika kila neno tumedhihirishwa kwenu.
2 Wakorintho 11:7 2ndCorinthians 11:7
Je! Nalifanya dhambi kwa kunyenyekea ili ninyi mtukuzwe, kwa sababu naliwahubiri Injili ya Mungu bila ujira?
2 Wakorintho 11:8 2ndCorinthians 11:8
Naliwanyang'anya makanisa mengine mali yao, nikitwaa posho langu ili niwahudumie ninyi.
2 Wakorintho 11:9 2ndCorinthians 11:9
Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
2 Wakorintho 11:10 2ndCorinthians 11:10
Kama vile ile kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, hakuna mtu atakayenifumba kinywa katika kujisifu huku, katika mipaka ya Akaya.
2 Wakorintho 11:11 2ndCorinthians 11:11
Kwa nini? Je! Ni kwa sababu siwapendi ninyi? Mungu anajua.
2 Wakorintho 11:12 2ndCorinthians 11:12
Lakini nifanyalo nitalifanya, ili niwapinge hao watafutao nafasi wasipate nafasi; ili kwamba katika neno hilo wajisifialo waonekane kuwa kama sisi.
2 Wakorintho 11:13 2ndCorinthians 11:13
Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.
2 Wakorintho 11:14 2ndCorinthians 11:14
Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
2 Wakorintho 11:15 2ndCorinthians 11:15
Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.
2 Wakorintho 11:16 2ndCorinthians 11:16
Nasema tena, mtu asidhani ya kuwa mimi ni mpumbavu; lakini mjaponidhania hivi, mnikubali kama mpumbavu; ili mimi nami nipate kujisifu ngaa kidogo.
2 Wakorintho 11:17 2ndCorinthians 11:17
Ninenalo silineni agizo la Bwana, bali kama kwa upumbavu, katika ujasiri huu wa kujisifu.
2 Wakorintho 11:18 2ndCorinthians 11:18
Kwa sababu wengi wanajisifu kwa jinsi ya mwili, mimi nami nitajisifu.
2 Wakorintho 11:19 2ndCorinthians 11:19
Ninyi, kwa kuwa mna akili, mnachukuliana na wajinga kwa furaha.
2 Wakorintho 11:20 2ndCorinthians 11:20
Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.
2 Wakorintho 11:21 2ndCorinthians 11:21
Nanena kwa jinsi ya kujidhili kana kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Walakini, akiwa mtu anao ujasiri kwa lo lote, (nanena kipuuzi), mimi nami ninao ujasiri.
2 Wakorintho 11:22 2ndCorinthians 11:22
Wao ni Waebrania? Na mimi pia. Wao ni Waisraeli? Na mimi pia. Wao ni uzao wa Ibrahimu? Na mimi pia.
2 Wakorintho 11:23 2ndCorinthians 11:23
Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.
2 Wakorintho 11:24 2ndCorinthians 11:24
Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.
2 Wakorintho 11:25 2ndCorinthians 11:25
Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;
2 Wakorintho 11:26 2ndCorinthians 11:26
katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang'anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;
2 Wakorintho 11:27 2ndCorinthians 11:27
katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.
2 Wakorintho 11:28 2ndCorinthians 11:28
Baghairi ya mambo ya nje, yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa yote.
2 Wakorintho 11:29 2ndCorinthians 11:29
Ni nani aliye dhaifu, nisiwe dhaifu nami? Ni nani aliyekwazwa nami nisichukiwe?
2 Wakorintho 11:30 2ndCorinthians 11:30
Ikinibidi kujisifu, nitajisifia mambo ya udhaifu wangu.
2 Wakorintho 11:31 2ndCorinthians 11:31
Mungu, Baba wa Bwana Yesu, aliye mtukufu hata milele, anajua ya kuwa sisemi uongo.
2 Wakorintho 11:32 2ndCorinthians 11:32
Huko Dameski liwali wa mfalme Areta alikuwa akiulinda mji wa Wadameski, ili kunikamata;
2 Wakorintho 11:33 2ndCorinthians 11:33
nami nikatelemshwa ndani ya kapu, katika dirisha la ukutani, nikaokoka katika mikono yake.