2 Wakorintho Mlango 2 2nd Corinthians
2 Wakorintho 2:1 2ndCorinthians 2:1
Lakini nafsini mwangu nalikusudia hivi, nisije kwenu tena kwa huzuni.
2 Wakorintho 2:2 2ndCorinthians 2:2
Maana mimi nikiwatia huzuni, basi ni nani anifurahishaye mimi ila yeye ahuzunishwaye nami?
2 Wakorintho 2:3 2ndCorinthians 2:3
Nami naliwaandikia neno lilo hilo, ili nijapo nisitiwe huzuni na wale ambao ilinipasa kuwafurahia; nikiwatumaini ninyi nyote kwamba furaha yangu ni yenu nyote pia.
2 Wakorintho 2:4 2ndCorinthians 2:4
Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilio nao kwenu jinsi ulivyo mwingi.
2 Wakorintho 2:5 2ndCorinthians 2:5
Lakini iwapo mtu amehuzunisha, hakunihuzunisha mimi tu, bali kwa sehemu (nisije nikalemea mno), amewahuzunisha ninyi nyote.
2 Wakorintho 2:6 2ndCorinthians 2:6
Yamtosha mtu wa namna hii adhabu ile aliyopewa na walio wengi;
2 Wakorintho 2:7 2ndCorinthians 2:7
hata kinyume cha hayo, ni afadhali mmsamehe na kumfariji, mtu kama huyo asije akamezwa katika huzuni yake ipitayo kiasi.
2 Wakorintho 2:8 2ndCorinthians 2:8
Kwa hiyo nawasihi kumthibitishia upendo wenu.
2 Wakorintho 2:9 2ndCorinthians 2:9
Maana naliandika kwa sababu hii pia, ili nipate bayana kwenu kwamba mmekuwa wenye kutii katika mambo yote.
2 Wakorintho 2:10 2ndCorinthians 2:10
Lakini kama mkimsamehe mtu neno lo lote, nami nimemsamehe; kwa maana mimi nami, ikiwa nimemsamehe mtu neno lo lote, nimemsamehe kwa ajili yenu mbele za Kristo,
2 Wakorintho 2:11 2ndCorinthians 2:11
Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.
2 Wakorintho 2:12 2ndCorinthians 2:12
Basi nilipofika Troa kwa ajili ya Injili ya Kristo, nikafunguliwa mlango katika Bwana,
2 Wakorintho 2:13 2ndCorinthians 2:13
sikuona raha nafsini mwangu, kwa sababu sikumwona Tito ndugu yangu, bali niliagana nao, nikaondoka kwenda Makedonia.
2 Wakorintho 2:14 2ndCorinthians 2:14
Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.
2 Wakorintho 2:15 2ndCorinthians 2:15
Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea;
2 Wakorintho 2:16 2ndCorinthians 2:16
katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo?
2 Wakorintho 2:17 2ndCorinthians 2:17
Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo.