Lyrics Page

Hadithi

By Guardian Angel

1,914 views Jun 6, 2026 updated

Hadithi hadithi njoo 

Hadithi hadithi njoo 

Hadithi hadithi njoo 


Verse 1

Kuna bwana mmoja wa kichaa  

alipenda kuomba chakula kwa mama fulani, mama fulani. 

Siku moja yule mama alipanga amtilie sumu, 

yule wazimu akila afe aondoke kabisa, 

kule njiani alipatana na watoto wa yule mama akawagawanyiaa kile chakula. 

Watoto wake wakala wakafa, yule wazimu akabaki mzima

ishara kwamba unayo yatenda unajitendea mwenyewe X 2

   

Chorus

Ukitenda mema unajitendea mwenyewe 

Ukitenda maovu unajitendea mwenyewe X 2


Verse 2 

Salimia watu pesa huisha 

Gari hupata puncture hivi ni vitu vya dunia, 

hichi kidole nacho wanyoshea watu. Vingine vinne ninajinyoshea mwenyewe X 2

Ninaozungumza nao juu ya wenzangu, wanazungumza nao juu yangu mimi X 2

Tenda mema ondoka uende alo na chuki na wewe mpende kwasababu unayo yatenda unajitendea mwenyewe*2 


Chorus

Ukitenda mema unajitendea mwenyewe 

Ukitenda maovu unajitendea mwenyewe X 2

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.